TTCL

EQUITY

Monday, April 25, 2016

Rais Magufuli ateua wa makatibu tawala wa mikoa

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 25 Aprili, 2016 amefanya uteuzi wa Makatibu Tawala wa Mikoa 26 ya Tanzania Bara.

Taarifa iliyotolewa leo na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa kati ya Makatibu tawala hao 10 ni wapya, 2 wamebadilishiwa vituo vya kazi na 13 wamebakisha katika vituo vyao vya sasa.

Makatibu Tawala wapya walioteuliwa ni kama ifuatavyo;
Arusha - Richard Kwitega
Geita - Selestine Muhochi Gesimba
Kagera - Armatus C. Msole
Kilimanjaro - Eng. Aisha Amour
Pwani - Zuberi Mhina Samataba
Shinyanga - Albert Gabriel Msovela
Singida - Dr. Angelina Mageni Lutambi
Simiyu - Jumanne Abdallah Sagini
Tabora - Dkt. Thea Medard Ntara
Tanga - Eng. Zena Said
Makatibu Tawala waliobadilishwa vituo vya kazi ni kama ifuatavyo;
Kigoma - Charles Amos Pallangyo (Kutoka Mkoa wa Geita)
Morogoro - Dkt. John S. Ndunguru (Kutoka Mkoa wa Kigoma)
Makatibu Tawala waliobakishwa katika vituo vyao vya sasa vya kazi ni kama ifuatavyo;
Dar es salaam -Theresia Louis Mbando
Dodoma - Rehema Hussein Madenge
Iringa - Wamoja Ayubu Dickolagwa
Katavi - CP Paul Chagonja
Lindi - Ramadhan Habibu Kaswa
Mara - Benedict Richard Ole Kuyan
Manyara - Eliakimu Chacha Maswi
Mbeya- Mariam Amri Mjunguja
Mtwara - Alfred Cosmas Luanda
Mwanza - CP. Clodwing Mathew Mtweve
Njombe - Jackson Lesika Saitabau
Rukwa - Symthies Emmanuel Pangisa
Ruvuma - Hassan Mpali Bendeyeko

Makatibu Tawala wa Mikoa 10 ambao wameteuliwa kwa mara ya kwanza, wataapishwa siku ya Jumatano tarehe 27 Aprili, 2016 saa tatu asubuhi Ikulu Jijini Dar es salaam.

No comments:

Post a Comment