TTCL

EQUITY

Monday, April 25, 2016

Mwigulu Nchemba atoa sababu 5 kilimo kuendelea TZ

Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mh. Mwigulu Nchemba ametoa sababu tano muhimu ambazo zinaweza kusaidia nchi kupiga hatua mbele kwenye kilimo na kusema moja ya hatua ni kuhakikisha watu wanaacha kilimo cha jembe la mkono kwa kuanza kutumia matrekta.
Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mh. Mwigulu Nchemba
Ili kukuza kilimo Mh. Nchemba amesema serikali inatakiwa kutengeneza mazingira ya kuunganisha mikoa kwa mifereji ili kuwezesha kilimo cha umwagiliaji ambacho kitakuwa hakina msimu wala hakitategemea mvua kama kilimo cha sasa ambacho kimekuwa kikitegemea mvua za msimu.
"Ili kilimo kiendelee Tanzania kinahitaji yafuatayo kwanza, kilimo cha kutumia Matrekta. Ni lazima kubadili mlinganyo uliopo wa watu wengi kutumi jembe la mkono kwenda watu wengi kutumia matrekta na kidogo kutumia Wanyama kazi. Jembe la mkono linatakiwa kuonekana Makumbusho ya Taifa yaani Museum na makaburini. Pili Kilimo cha Umwagiliaji, lazima serikali kuunganisha Mikoa kwa mifereji ya Umwagiliaji ili wakulima wayatoe maji kwenye hiyo mifereji kwenda mashambani mwao, pana safari ndefu hapa," alisisitiza Mwigulu Nchemba
Lakini mbali na hayo alizidi kutoa ufafanuzi kuwa matumizi ya pembejeo ni muhimu katika kufanya kilimo na zinatakiwa kupatikana popote nchini na kwa watu wote masikini na matajiri kama ambavyo watu wanaweza kununua vinywaji baridi.
"Matumizi ya Pembejeo, ni lazima mbolea, mbegu bora na dawa zipatikane madukani kama sodaa inayopatikana popote na kwa wakati, kwa tajiri na masikini na kwa bei ya kumudu kila mtu. Nne Lazima yawepo maghala na viwepo viwanda kwa ajili ya kuyapokea mazao haya kwa kila zao lichakwatwe na kupata by product, mfano kwa pamba tupate nguo hapa hapa nchini, kwa ngozi tupate viatu na mikanda, begi hapa hapa, matunda tupate juisi hapa hapa nk ili kuondoa post harvest loses.
Mbali na hayo Mwigulu Nchemba alisema kuwa tunahitaji kuwa na wataalam wa kutosha wa kilimo pamoja na vyuo imara vyenye kutoa wataalam makini na kuwa na vyuo vya utafiti ambavyo kazi yake kubwa itakuwa kufanya takwimu mbalimbali zenye kulenga tija katika kilimo chini.
"Tano Lazima tuwe na wataalam na uimara wa vyuo vya utafiti. Lazima wakulima walime kwa kufuata utaalam. Kwa Mifugo lazima tuwe na mitambo ya mifugo wa kisasa wa maziwa na nyama ili kupata tija kubwa kutokana na kundi dogo. Lazima tuwe na maeneo ya malisho ambayo mifugo itakaa kwa uwiano wa kitaalam huku na huduma kama maji, majosho na wataalam yakipatikana hapo katika ufuagaji wa kibiashara, " alisisitiza Mwigulu Nchemba.

No comments:

Post a Comment