TTCL

EQUITY

Wednesday, January 20, 2016

Mwili wa Mbunge Leticia Nyerere wawasili jijini Dar mazishi yake kufanyika Butiama mkoani Mara kesho

Askari wa Bunge wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mara, Leticia Nyerere aliyefariki nchini Marekani alikokuwa akitibiwa mara baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam jana jioni. Mwili huo leo utaagwa nyumbani kwa Mwalimu Nyerere Msasani kabla ya kusafirishwa kwenda Butiama mkoani Mara kwa mazishi yatakayofanyika kesho.

Mwili huo ukiingizwa kwenye gari maalumu katika uwanja huo.

Ndugu jamaa na marafiki wakijadiliana jambo wakati wa kuupokea mwili huo.

Ndugu, jamaa, marafiki na watoto wa marehemu wakisubiri kuupokea mwili wa mpendwa wao.

Mume wa marehemu, Madaraka Nyerere akizungumza na wanahabari baada ya kuupokea mwili huo uwanjani hapo.

Mtoto wa marehemu (kulia), akifarijiwa na mmoja wa ndugu wakati wakienda kupanda gari kabla ya kuondoka uwanjani hapo.

DSC_1000
Rais wa Simba, Evans Aveva akizungumza na wanahabari akiwemo mwanahabari wa mtandao huu Rabi Hume (kulia) katika eneo la makaburi ya Kisutu jana 18 Januari. ambapo amemuelezea marehemu aliyekuwa mwanachama wa muda mrefu wa Simba na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini, Mhandisi Suleiman Said kuwa alikuwa nguzo muhimu.

Rais wa Simba, Evans Aveva na mbunge wa zamani wa Kinondoni, Idd Azan wamezungumzia kifo cha aliyekuwa mwanachama wa muda mrefu wa Simba na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini, Mhandisi Suleiman Said na kumtaja kuwa moja ya nguzo muhimu ndani ya Simba na taifa ambaye nafasi yake ni ngumu kuzibika.
Akizungumza na Mo Dewji Blog, Rais wa Simba, Evans Aveva amesema kifo cha Suleiman kimekuwa cha kushtusha ndani ya Simba na kifo chake kimekuwa ni pigo kubwa kwa wadau wa soka nchini kwa kupoteza mtu muhimu katika soka la Tanzania.
Aveva amesema Suleiman alikuwa akisifika kwa msimamo wake na hivyo kujipatia heshima kubwa katika soka la Tanzania lakini pia kuwa mtu mwenye mchango mkubwa katika klabu ya Simba na kwake binafsi amepoteza mwalimu wake katika uongozi wa soka.
“Kifo cha Suleiman kimekuja kwa kutushtukiza kwa wana Simba na hata kwa mimi kama kiongozi wa Simba, alikuwa na mchango mkubwa katika klabu ya Simba na hata kwa soka la Tanzania kiujumla na pengo lake itakuwa ngumu kuja kuzibika,
“Suleiman alikuwa anasifika zaidi kwa msimamo wake ulikuwa hauteteleki na kwangu binafsi nimepoteza mwalimu na yeye ndiyo aliyenipokea wakati naanza kuingia katika mambo ya uongozi ndani ya Simba,” alisema Aveva.
Aidha Aveva aliongeza kuwa tayari klabu ya Simba imeshatoa rambirambi ya 500,000 na uongozi unataraji kuzungumza kuona ni jinsi gani watamuenzi Suleiman ambaye aliwahi kuwa kiongozi wa Simba.
Nae mbunge wa zamani wa Kinondoni na mwanachama wa muda mrefu wa Simba, Idd Azzan amemtaja Suleiman kama kiongozi bora kutokana na kupenda kujenga umoja baina ya wanasimba na alikuwa na msimamo ambao uliifanya Simba kuonekana timu bora hata kama mambo hayakuwa sawa.
Alisema kuwa Suleiman alikuwa mchapakazi na mwenye roho ya ukarimu mambo ambayo yatamfanya kuwa akimkumbuka kwa wakati wote kutokana na tabia zake hizo ambazo ziliisaidia Simba na taifa kwa ujumla kwa kipindi ambacho alikuwa mkurugenzi wa viwanja vya ndege nchini.
“Alikuwa ni kiongozi ambaye alikuwa akijenga umoja kwa wanasimba na hakukubali kuwa na makundi na ndani ya klabu na jambo hilo lilikuwa linaisaidia Simba kupata matokeo mazuri kutokana na mshikamano alioujenga,
“Ni pigo kwa Simba kupoteza mwanachama wa muda mrefu wa Simba na taifa kwa kupoteza mchapa kazi aliyekuwa akiwa ni Mkurugenzi wa Viwanja vya Ndege Tanzania na katika kazi yake alikuwa mchapa kazi sana alikuwa ana mipango mingi na maeneo mengi ameyasaidia kupata viwanja vya ndege,” alisema Azzan.
DSC_0988
Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Kinondoni, Mh. Idd Azzan akisalimiana na baadhi ya wanachi waliofika kwenye makaburi ya Kisutu katika mazishi hayo.
DSC_1007
Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Bwana Richard Kasesela akisalimiana na wananchi wengine waliofika katika mazishi hayo katika makaburi ya Kisutu.
DSC_0981
NaibuWaziri wa Afya Zanzibar, Bwana Mahmoud Thabit Kombo (alievaa kanzu na miwani) akisalimiana na watu mbalimbali waliofika kwenye mazishi hayo.

No comments:

Post a Comment