Mke wa Rais wa Zamani wa Kenya, Mama Lucy Kibaki (pichani) amefariki dunia nchini Uingereza katika hospitali ya Bupa Cromwell alipokuwa akipatiwa matibabu, taarifa hizo zimethibitshwa na Rais Uhuru Kenyatta ambapo amesema aliugua kwa zaidi ya mwezi mmoja na alikuwa akipatiwa matibabu Kenya kabla ya nchini Uingereza kwa tiba zaidi.
Rais Uhuru Kenyatta amesema katika taarifa yake hiyo Mama Kibaki, atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa kwenye maendeleo ya nchi na hasa alivyosaidia katika mapambano dhidi ya Ukimwi
Unboundaries News: Inatoa pole kwa ndugu, familia ya marehemu na Wakenya wote kufuatia msiba huu mkubwa na Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema Ameen.!