TTCL

EQUITY

Tuesday, April 26, 2016

Serikali kuendelea kufanya tathmini ya Viwanda

Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Msajili wa Hazina, inafanya ufutaliaji na tathmini katika viwanda na mashirika ya Umma yaliyobinafsishwa ili kubaini kama mikataba waliyoingia inafuatwa au la ili kuchukua hatua stahiki.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage
Akizungumza jana bungeni katika kipindi cha maswali na majibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage, amesema mikataba yote ya mauzo inapitiwa endapo itabainika kuwa imekiuka mashariti hatua za kisheria zitakuchukuliwa ikiwemo serikali kuvirejesha viwanda hivyo.

Mhe. Mwijage, amesema kuwa viwanda ambavyo vitaonekana wamiliki wanauwezo wa kuvifufua makubaliano mapya yatafikiwa huku akiongeza kuwa wawekezaji wenye nia ya kuwekeza nchini watatafutwa.

Aidha Waziri huyo wa Viwanda amesema kuhusu viwanda ambayo vimebainika kuwa havifanyi kazi wanavifatilia kwa kuangalia ubinfsishaji wa kisheiria ili kuvirejesha mikoni mwa serikali kisheria ili kuepuka migangano ambayo inaweza kujitokeza.

Mhe. Mwijage ameongeza kuwa kwa viwanda ambavyo vilibinafsishwa kwa wawekezaji wazawa watawafata ili wasaidiane nao kujua changamoto zinazowakabili kufanya uzalishaji na kuwasaidia waweze kuvifufua viwanda vyao.

Pia ameongeza kuwa serikali inaendelea kufanya jitihada za kudhibiti uingizwaji wa bidhaa za nje zisizo na ubora ili bidhaa zinazozalishwa katika viwanda vya ndani viweze kupata masoko bora ya bidhaa zao.

No comments:

Post a Comment