
Kwa mujibu wa ripoti hiyo jumla
ya watu 14,105 wameugua na kati yao 218 wamepoteza maisha nchini na
bado ugonjwa huo upo katika mikoa ya Kilimanjaro, Lindi, Arusha,
Morogoro,Simiyu,Mwanza,Rukwa na Dar es salaam.
Kipindupindu
ni miongoni mwa magonjwa ambayo husababishwa na aina ya bakteria
aitwaye Vibrio cholerae, Ugonjwa huu ni wa kuambukizwa kwa njia ya viini
vinavyoenezwa kupitia kwa kinyesi kutoka kwa wagonjwa wenye
Kipindupindu.

Vile
vile sababu kubwa sana ya ugonjwa huu ni pamioja na Mabomba ya kupitisha
maji machafu yasiyofunikwa na matanki ya maji ya kunywa yasiyofunikwa
huchangia katika kusababisha mkurupuko wa kipindupindu.
Baada ya
Rais John Magufuli kuifanya tar 09 Desemba2015 kusheherekea Uhuru kwa
kufanya usafi na Serikali kutangaza kila jumamosi ya mwisho wa mwezi
kuwa siku ya usafi lakini kama watendaji hawatasimamia matamko yao kwa
dhati na kwa kuzingtia nguvu kazi na vifaa kwa ajili ya kufanyia usafi
bado ugonjwa huu utasumbua sana.
Ni
dhahiri kwamba jitihada zaidi zinahitajika katika miji yetu kukabili
ugonjwa huu hasa uzoaji taka, katika miji yetu bado ni wa
kusuasua,madampo ya kuhifadhia taka nayo ni kero kila kona, mifereji na
mabomba ya maji taka lazima yatazamwe kwa jicho jingine kwani katika
maeneo mengi hasa ya jiji la Dar es salaam chemba nyingi zinavujia
barabarani ,usafi wa mazingira ni vyema uwe ajenda ya kila mwananchi.
No comments:
Post a Comment