TTCL

EQUITY

Tuesday, December 15, 2015

KAPUMZIKE KWA AMANI MPAMBANAJI MWENZETU DOTTO MZAVA.

BLOGGER chipukizi nchini Dotto Mzava, amefariki Dunia katika ajali ya barabarani Desemba 14, 2015 Jijini Dar es Salaam. 
Kwa mujibu wa taarifa ya Mwenyekiti wa Mtandao wa Bloggers Nchini, (TBN), ambao marehemu alikuwa ni mwanachama wake, Bw. Joackim Mushi amesema Dotto ambaye alikuwa akifanyia kazi Jamii Media (Wamiliki wa mtandao wa Jamii Forum) amapo pia alikua akimiliki tovuti yake ya Fikra pevu, Marehemu amefariki kwa ajali ya pikipiki ingawa haikuelezwa ajali hiyo imetokea maeneo gani hasa ya jiji la Dar es Salaam.
Bwana ametoa na Bwana ametwaa Jina lake Lihimidiwe Amin.

No comments:

Post a Comment