TTCL

EQUITY

Thursday, November 6, 2014

Staa wa bongofleva aliebadili dini, sababu na jina lake jipya viko hapa…

Hafsa1
Star wa hit single ya Presha Hafsa Kazinja ambayo alishirikishwa mkali mwingine kutoka B Band Banana Zoro November 06 ameiteua kuwa siku rasmi ya kuwafahamisha mashabiki wake na watu wake wa karibu kuhusu jina lake jipya analotumia kwa sasa.
Hafsa ambaye tangu aanze kujihusisha na kanisa ni miezi 10 kwa sasa, November 05 2014 ameamua kubatizwa rasmi na kuwa Mkristo kutoka kwenye dini yake ya awali.
Kwa sasa anaitwa Christina Kazinja na amebatizwa katika kanisa la Zoe Christy Ministrylililopo Tabata Segerea Dar es salaam na hii ni baada ya matatizo aliyoyapata na kusema kuwa kaona Yesu ndiye mkombozi wa maisha yake kwa sasa.
Hafsa Kazinja ni miongoni mwa mastaa wachache wa Tanzania waliokuwa wakitumia majina yao halisi kwenye kazi zao za sanaa na hivyo kwa kubadilisha kwake dini inamaanisha na jina limebadilika, atatumia Christina Kazinja.

No comments:

Post a Comment