TTCL

EQUITY

Monday, January 25, 2016

Mitaala ya somo la uraia na maadili kuanza kutumika mwaka huu

 
Mkurugenzi wa ubunifu na uboreshaji mitaala katika Taasisi ya elimu nchini nchini Dkt. WILBERFORCE MEENA amesema mitaala ya somo la uraia na maadili itaanza kutumika mwaka huu.

Mkurugenzi wa ubunifu na uboreshaji mitaala katika Taasisi ya elimu nchini nchini   Dkt. WILBERFORCE MEENA amesema  mitaala ya somo la uraia na maadili itaanza kutumika mwaka huu kwa elimu ya msingi na sekondari  kwa lengo la kuzalisha wataalam watakaoisambaza elimu hiyo kwa jamii.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina ya mafunzo kwa viongozi wa dini  nchini Dkt. MEENA amesema elimu hiyo itasaidia kupatikana kwa wataalam bora wa utatuzi wa migogoro nchini.

Kwa upande wake  Mkurugenzi wa Baraza la Dini mbalimbali nchini  Mchungaji CONON GODDA amesema lengo la semina hiyo ni kuelezana jinsi ya kukaa pamoja na kutatua migogoro kwa njia ya mazungumzo na kuandaa wataalamu watakaotoa elimu ya amani katika jamii.

No comments:

Post a Comment