TTCL

EQUITY

Friday, March 25, 2016

RAIS MAGUFULI ATOA ZAWADI ZA PASAKA

Rais John Pombe Magufuli amekabidhi zawadi zenye jumla ya shilingi milioni tisa kwenye vituo ishirini na nne vya watoto wa mitaani.
 
Kaimu Kamishna Msaidizi wa Ustawi wa Jamii Rabikira Mushi akizungumza na waandishi wa habari kabla ya kukabidhi zawadi za Pasaka zilizotolewa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh John Pombe Magufuli.

Rais Magufuli amekabidhi zawadi zenye jumla ya shilingi milioni tisa kwenye vituo ishirini na nne  vya watoto wa mitaani pamoja na wazee nchi nzima katika kuadhimisha sikukuu ya Pasaka.
Akikabidhi zawadi hizo kwa niaba ya Rais Kaimu Kamishna Msaidizi wa Ustawi wa Jamii Mushi amesema kuwa zawadi hizo kutoka kwa raisi ni salamu zake kwa watoto wa mitaani wasiojiweza pamoja na wazee.

Naye mmoja wa wasimamizi wa kituo cha Nyumba ya Furaha na Amani kilichopo Mburahati Sister Innocensia Kagoma na mmoja wa watoto wanaolelewa katika moja ya vituo vya  kulea watoto cha Mbweni amemshukuru Rais Magufuli kwa zawadi hizo na kutoa wito kwa wadau wengine kuwa na moyo wa kusaidia watu wenye uhitaji.

No comments:

Post a Comment