Wasanii
kutoka nchini China wakionyesha umahiri wao wakati wa Tamasha la
Jifunze Utamaduni wa China lililofanyika jana jijini Dar es Salaam,
ambao makundi mbalimbali ya china yalitoa burudani za aina mbalimbali ya
michezo jukwaani.
Mkurugenzi
wa Idara ya Habari (MAELEZO) Assah Mwambene (kulia) akikaribishwa na
Balozi wa China nchini Tanzania Lu Youqing (kushoto) allipohudhuria
hafla ya Tamsaha la Jifunze Utamaduni wa China lililofanyika jana
jijini Dar es Salaam.
Katibu
Mkuu wa Wizra ya Nishati na Madini Eliakim Maswi, akitoa hotuba yake
wakati wa onyesho la tamasha la jifunze utamaduni wa China katika
Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijijni Dar es Salaam, ambapo aina za
michezo mbalimbali pamoja na nyimbo, mazingaombwe kutoka kikundi cha
Utamaduni cha Taifa kutoka China kilionyesha na kutoa burudani safi kwa
wageni waliohudhuria.
Kikundi cha Utamaduni cha Taifa kutoka China kikionyesha sanaa yao jukwaani.
Sehemu ya wageni waalikwa wakifuatilia tamasha hilo.
Kikundi cha utamaduni kutoka Tanzania kikitoa burudani, jukwaani.
No comments:
Post a Comment