TTCL

EQUITY

Monday, April 25, 2016

LHRC serikali iweke mfumo wakutatua matatizo

Mkurugenzi wa LHRC Dkt. Hellen Kijo - Bisimba
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu nchini Tanzania (LHRC) kimeitaka serikali kuweka mfumo maalum wa kushughulikia matatizo ndani ya nchi.
Mkurugenzi wa LHRC Dkt. Hellen Kijo-Bisimba ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na East Africa Television na East Africa na kuainisha kuwa ni lazima kuwe na mfumo maalum ambao utaweza kusaidia mambo yaende kwa kufuata sheria na Katiba ya nchi ilinavyoelekeza.

 
Amesema Rais Dkt John Pombe Magufuli ameanza kutekeleza mambo ambayo makundi ya kutetea haki za binaamu waliyapigania kwa miaka mingi na hayakuweza kutekelezwa kwa wakati huo kutokana na kuwepo kwa usimamizi mbovu kwa baadhi ya sekta mbalimbali nchini hivyo ni vema kuwa na uangalifu wa hali ya juu katika utekelezaji wake.

Amesema kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kinamuunga mkono rais Dkt. Magufuli na kituo cha LHRC kina nia njema na wananchi wa Tanzania pamoja na serikali yake ndiyo maana kituo kimekuwa mstari wa mbele kusimamia haki itendeke kwa kuzingatia mfumo na utawala wa sheria ya nchi inavyoelekeza.

 
Kwa upande mwingine Dkt. Kijo - Bisimba amesema kitendo kinachofanywa na kambi ya upinzani Bungeni cha kutoka kwenye baadhi ya vikao vya Bunge ni aina mojawapo ya uwasilishwaji wa jambo fulani hivyo ni lazima wanasiasa watumie njia ya Kidemokrasia katika kuwatumikia wananchi wake.

No comments:

Post a Comment