Rais
JOHN MAGUFULI amemtembelea Waziri Mkuu Mstaafu FREDERICK SUMAYE ambaye
amelazwa katika Hospitali ya Taifa MUHIMBILI jijini DAR ES SALAAM
Rais
Dkt John Pombe Joseph Magufuli akimpa pole Waziri Mkuu Mstaafu Mhe
Freredick Sumaye alipokwenda kumjulia hali katika Taasisi ya Moyo ya
Jakaya Kikwete katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es
salaam leo Jumatatu Januari 11, 2016
Rais JOHN MAGUFULI amemtembelea Waziri Mkuu Mstaafu
FREDERICK SUMAYE ambaye amelazwa katika Hospitali ya Taifa MUHIMBILI
jijini DAR ES SALAAM, katika Taasisi ya Moyo ya JAKAYA KIKWETE.
Katika mazungumzo yao SUMAYE amemsifu Rais MAGUFULI kwa kuwajali watanzania bila kuangalia itikadi zao za vyama.
Katika hatua nyingine, Rais MAGUFULI amekwenda nyumbani kwa Hayati
Baba wa Taifa Mwalimu JULIUS NYERERE kumpa pole Mama MARIA NYERERE
kufuatia kifo cha LETICIA NYERERE aliyefariki dunia akiwa nchini
MAREKANI.
LETICIA NYERERE alikuwa mbunge wa viti maalum katika bunge la 10 lililomalizika mwaka 2015.
No comments:
Post a Comment