TTCL

EQUITY

Thursday, December 24, 2015

Polisi yadhibiti ongezeko la nauli ya mabasi ya mikoani na uuza tiketi bei ya juu.

Jeshi la Polisi kikosi cha usalama barabarani linawashilikia makondakta na mawakala wa mabasi mbalimbali yanayofanya safari zake mikoani kwa kosa la kuuza tiketi za kusafiria kwa bei ya juu kinyume na sheria ambapo wakati hao wakiwa wanashikiliwa maelfu ya abiria wameshindwa kusafiri kutokana na kutokuwepo kwa mabasi ya kutosha.

ITV imefika kituo cha mabasi Ubungo na kushuhudia idadi kubwa ya  abiria wakiwa hawajui nini cha kufanya kutoka na kukosa usafiri ambapo wengine wamelazimika kusitisha safari zao na wegine wakidai kuwa wamiliki wa mabasi wamebadilisha safari za mabasi yao ndio maana usafiri umekuwa mgumu.
Akijibu tuhuma hizo msemaji wa chama cha wamiliki wa mabasi TABOA Bw Mustaph Mwalongo amesema siyo kweli kuwa mabasi yamebadilisha safari bali magari mengi yameenda mikoani na yanashindwa kurudi kwa sababu hakuna abiria wengi wanaokuja Dar es Salaam.
Wakati hali hiyo ikitokea mkuu wa kikosi cha usalama barabarani kamanda Mohamedi Mpinga amesema wapo watu ambao wanashikiliwa kwa mahojiano zaidi kwa kosa la kuuza tiketi kwa bei ya ulanguzi na watachukuliwa hatua za kisheria muda wowote uchunguzi ukishakamila.
Aidha ITV ikiwa kituoni hapo kilishudia kondakta wa basi la Abood  lenye namba za usajili T 517 AGD linalofanya safari zake kati ya Dar na Iringa akiwa mikononi mwa polisi kwa kosa la kuuza tiketi kwa bei ya juu.

No comments:

Post a Comment