TTCL

EQUITY

Thursday, December 24, 2015

Baadhi ya wananchi wameiunga serikali mkono mpango wa kutoa elimu bure kwa kutoa madawati milioni 1 na nusu.

Ikiwa ni katika kuunga mkono jitihada za serikali za kutoa elimu bure baadhi ya wanachi ambao ni wazawa wameunga mkono mpango huo kwa kutoa madawati milioni moja na nusu bure kwa shule ambazo  zitakuwa hazina madawati hatua ambayo itaipunguzia serikali gharama za kununua madawati na fedha hizo kuelekezwa katika mambo mengine  yanayohusu elimu.

Wakizungumza jijini Dar es Saalam baadhia ya watu waliojitolea kutoa madawati wamesema wameguswa na jihada nzuri zinazofanywa na rais Dk John Magufuli za kuinua kiwango cha elimu bure na hivyo wanaona ni busara kuunganisha nguvu.
 
Naye bw oscar kaduma amesema kupitia rasilimali za mbao zilizopo nchini wameona ni vyema wakatumia rasilimali hizo kuutengneza madawati amabyo yatawasaidia wanachi wa kawaida amabo kwa miaka mingi sana wamekuwa wakipata shida kwa watoto wao kukaa chini.
 
Hatua hiyo imeungwa mkono na baadhi ya wazazi na wanaharakati wa elimu nchini na ambapo wamesema watoto wamekuwa wakikaa chini kwa muda mrefu  hatua ambayo ilikuwa inawafanya washindwe kufanya vizuri katika masomo yao.

No comments:

Post a Comment