HALI
isiyokuwa ya kawaida Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza, limekiuka sheria
na kuanza kupiga mabomu ya macho katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando
(BMC), kuwatawanya wafuasi wa Chadema.
Tukio hilo limetokeaza leo jioni, baada ya
wafuasi hao kuanza mvutano na askari Polisi mmoja na ndipo vurugu
zilizodumu kwa saa moja na nusu.
Hata hivyo wafuasi hao kabla ya kuanza vurugu hizo, walizima kuruka kuta za hospitali na kufungua geti kwa mabavu.
Chombo chetu cha habari kilishuhudia Polisi huyo na wafuasi wa Chadema wakivutana nje ya mlango wa vyumba vya kuhifadhi maiti.
Baada ya mvutano huo wafuasi hao wa Chadema walianza kumuangushia
kichapo askari huyo ambaye anatuhumiwa kufanya njama za kurudisha mwili
wa marehemu mkoani Geita kwa madai kwamba tukio lilitokea huko.
Hali hiyo ya askari kuangushiwa kichapo, lilikuja gari la polisi
ambalo lilikuwa na polisi ambao walikuwa na mabomu ya machozi na silaha
za moto na kuanza kipiga mabomu.
Aidha Mwandishi wa habari hizi, alishuhudia Polisi mmoja akimpiga
mjane wa marehemu, katika vurugu hizo ambazo zilianzishwa na polisi
wenyewe ambao walilazimisha kuingia kwenye chumba hicho.
Katika vurugu hizo, polisi walimtia mbaroni Mwenyekiti wa Bavicha Taifa, Pastrobas Katambi na baadhi ya wafuasi zaidi ya wanne.
Awali wakati wafuasi wa Chadema wakiupokea mwili wa marehemu,
walikuwa walisikika wakiimba, “Kama sio wewe Mkapa na mauaji yangetoka
wapi.”
Hata hivyo wafuasi hao ambao waliupokea mwili wa marehemu katika
kivuko cha Busisi ambapo walipofika kati kati ya Jiji la mwanza
walitokea wafuasi wengine ambao walikuwa nao walisikika wakiimba,” CCM
wameua CCM wameua… Hadi katika BMC.
Kifo cha Mawazo kinahusishwa na mmoja wa viongozi wakubwa wa CCM Mkoa
wa Geita, ambaye ni mmiliki wa mabasi yanayofanya safari zake Mwanza –
Geita.
Kuhusishwa kwa kigogo huyo wa CCM na kifo hicho, inadaiwa kuwa gari
lake lilionekana likiwabeba vijana wanaotajwa kuhusika na mauaji hayo na
kuwaleta mjini hapa.
Pia kigogo huyo ambaye ni Mbunge mteule wa kati ya majimbo ya mkoa
huo, anahusishwa kuandaa mtandao wa wauaji hao ambao mmoja wao anadaiwa
kutoka jijini hapa.
Pia Mawazo ambaye alikuwa ni mgombea ugunge jimbo la Busanda
akichukuana na Lolencia Bukwimba (CCM) inadaiwa alikuwa anatarajiwa
kwenda mahakamani kupinga ushindi wa Bukwimba.
Hata hivyo inaelezwa kuwa endapo kama
marehemu angefungua mashtaka polisi angeshinda kesi kutokana na
ushahidi wa video zinazowaonesha polisi kuwatisha mawakala wa Chadema
kusaini matokeo kwa lazima.
Akizungumza na wafuasi wa Chadema, Godbless Lema, amesema kifo cha
Mawazo ni mpango wa Chama cha Mapinduzi na kulitaka Jeshi la Polisi
kuwakamata watu wanaohusishwa na kifo hicho.
No comments:
Post a Comment