mafundisho ya afya ya uzazi laendelea mkoani iringa.
Pichani ni Muuguzi wa UMATT,Bi.Mery Biseko akionesha
namna ya kutumia Kondom za kike kwa vijana mbalimbali (hawpao pichani) waliojitokeza katika tamasha la mafundisho ya afya ya uzazi yanayoendelea katika viwanja vya Kihesa sokoni,mkoani Iringa.
Mratibu
wa mradi wa TUWALEE kutoka katika shirika la UMATT,Bi Jemida Kulanga,
akitoa elimu ya Afya ya Uzazi kwa vijana mbalimbali waliokuwa
wamejitokeza katika tamasha la mafundisho ya afya ya uzazi yanayoendelea
katika viwanja vya Kihesa sokoni,mkoani Iringa.
======== ======= =======
Shirika
la UMATT linakabiriwa na changamoto ikiwemo ya kutokuaminika katika
huduma wanazotoa, hasa katika suala la upimaji afya kwa wateja wao na walio
wengi hawana elimu juu ya afya ya uzazi.
Hayo yamesemwa na Mratibu wa mradi wa TUWALEE kutoka katika
shirika hilo,Bi Jemida Kulanga, wakati akizungumza na wandishi wa habari katika
tamasha la mafundisho ya afya ya uzazi yanayoendelea katika viwanja vya Kihesa
sokoni,mkoani Iringa.
Bi.Jemida amesema kuwa kuna haja kubwa ya kutoa elimu ya afya ya
uzazi kwa vijana ambapo itasaidia kupunguza magonjwa mbalimbali yatokanayo na
ngono pamoja na mimba zisizotarajiwa .
Amesema kuwa wameamua kufanya tamasha hilo kutokana na asilimia kubwa ya
wateja wao waliofika katika ofisi zao ,wameonekana kuwa na uelewa mdogo juu ya
afya ya uzazi ikiwemo matumizi ya mpango wa uzazi.
Hata
hivyo katika mafunzo hayo pia wameweza kufundisha matumizi ya Kondomu za kike
kwa wanawake ,kwani wanawake wengi wameonekana kutokujua matumizi yake na
wengine kutokuijua kabisa kondom hiyo ya kike.
Aidha amewataka vijana kutafuta habari zinazohusu afya ya uzazi
ili kuepuka magonjwa hatarishi yanayohusiana na suala zima la uzazi.
No comments:
Post a Comment