TTCL

EQUITY

Tuesday, January 12, 2016

Wajumbe kamati ya kanuni za bunge wateuliwa

Spika wa Bunge JOB NDUGAI ameteua wajumbe wa Kamati ya Kanuni za Bunge ambayo inaundwa na wabunge 15
 
Spika wa Bunge Job Ndugai
 
Spika wa Bunge JOB NDUGAI ameteua wajumbe wa Kamati ya Kanuni za Bunge ambayo inaundwa na wabunge 15.
Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Bunge jijini Dar Es Salaam imesema kamati hiyo inatakiwa kufanyia marekebisho ya nyongeza ya NANE ya kanuni za kudumu za bunge, kuhusu majukumu ya kamati zingine za bunge ili kuendana na majukumu ya serikali kwa kuzingatia muundo wa Baraza la Mawaziri.
Kamati hiyo inaundwa na Spika wa Bunge ambaye anakuwa mwenyekiti na makamu wake ni Naibu Spika, huku Kiongozi wa Upinzani na Mwanasheria Mkuu wa Serikali wakiwa wajumbe kwa nyadhifa zao.
Wajumbe wengine walioteliwa na Spika ni  MAKAME KASSIM MAKAME, TUNDU LISSU, JASSON RWEIKIZA, ALLY SALEH ALLY, MAGDALENA SAKAYA, SALOME MAKAMBA, Dkt. JASMINE BUNGA, ZAINAB KATIMBA, Balozi ADADI RAJAB, Dkt. CHARLES TIZEBA na KANGI LUGOLA.
Wajumbe hao wanatakiwa kukutana tarehe 15 mwezi huu jijini Dar Es Salaam.
Taarifa hiyo imesema Spika atakamilisha uteuzi wa Wajumbe katika Kamati zingine za Bunge kabla ya kuanza kwa mkutano wa pili wa Bunge unaotarajiwa kuanza tarehe 26 mwezi huu.

No comments:

Post a Comment