Kutokana na uzuri wa eneo hili kimalisho kabila la wamasai na wameru waliweka makazi kwa sababu ya uhakika wa chakula cha mifugo yao.
Baada ya mji huu kuwa eneo maarufu la malisho idadi ya watu iliongezeka na shughuli mbalimbali haswa za kibiashara zikaanza ambapo ziliweza kuvutia Wakoloni.
Wakoloni wa kwanza kuja Arusha ni wajerumani ambapo waliwatanguliza wamishionari lengo likiwa ni kutaka kutwaa eneo hili na kuwa makoloni yao.
Waarusha hawakukubali kutawaliwa kirahisi na waliweza
kupigana na wamishenari hao na kuwaua. Hata hivyo baadae kidogo
Wajerumani walikuja tena na kupigana vita na Mangi wa Arusha
Lavaito/Meingeanga Ndemi mwaka 1890-1900.
No comments:
Post a Comment