TTCL

EQUITY

Wednesday, November 11, 2015

Tanzania hatarini kukabiliwa na uhaba wa maji

Tanzania ni moja ya nchi za ukanda wa bahari ya Hindi ambazo zinatabiriwa kuwa huenda zikakabiliwa na uhaba wa maji pamoja na ongezeko la bei za vyakula kutokana na athari za mabadiliko ya hali ya hewa zinazoendelea kujitokeza na kuathiri sekta mbali.

Meneja Takwimu za Hali ya Hewa nchini ,Janet Loning`o
Hayo yameelezwa na meneja takwimu za hali ya hewa nchini , Janet Loning`o akizungumza katika warsha ya mafunzo juu ya takwimu za hali ya hewa kwa nchi za bahari ya Hindi pamoja na mataifa ya Ulaya inayoendelea jijini Arusha ,
Lining'o amesema kuwa licha ya uhaba wa maji pia mabadiliko ya hali ya hewa yanachangia kiasi kikubwa ongezeko la joto hivyo wananchi wanapaswa kupewa elimu juu ya kukabiliana na athari zinazotokana na mabadiliko ya hali ya hewa.
Meneja huyo amesema kuwa wanajifunza kufanya uokoaji wa takwimu za hali ya hewa ambazo bado hazijaingizwa kwenye mfumo wa digitali kwani ni za miaka mingi iliyopita na zinasaidia katika kutabiri iwapo kuna uwezekano wa kutokea kwa ukame na mafuriko katika maeneo mbalimbali nchini.
Msaidizi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini Kenya, Peter Ambenje Amesema kuwa uhifadhi huo wa takwimu utasaidia kuzuia upotevu wa takwimu muhimu katika masuala ya mabadiliko ya hali ya hewa.
Mabadiliko ya hali ya hewa ni tatizo linaloikumba dunia na kusababisha madhara mbalimbali ikiwemo ukame, ongezeko la joto na uhaba wa maji huku nchi nyingi za Afrika zikiwa ni wahanga wakubwa wa mabadiliko hayo, juhudi za kupanda miti na kutunza mazingira zinapaswa kuchukuliwa haraka ili kunusuru dunia na mabadiliko ya hali ya hewa.

No comments:

Post a Comment