TTCL

EQUITY

Thursday, June 27, 2013

Wataka wajumbe wa baraza Z’nzibar wasilipwe posho

Pemba: Chama cha UDP Zanzibar kimeitaka Serikali kutowalipa posho wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar na kuwapunguzia mshahara wajumbe ambao hawachangiikatia vikao vya baraza hilo. 

Kauli hiyo ilitolewa na Naibu Katibu wa UDP Zanzibar, Juma Khamis Faki wakati akizungumza na gazeti hili baada ya kubaini kuna baadhi ya wajumbe wa baraza ambao kazi yao ni kusinzia wakati wakiwa barazani .

Alisema kutolipwa posho kwa wajumbe hao pamoja na kukatwa kwa mishahara yao itakuwa ni fundisho kwa wale wasio na kawaida ya kuchangia hoja pamoja na kuwatetea wananchi
waliowachagua .
Alibainisha kuwa vitendo vya viongozi hao wa majimbo kushindwa kuchangia hoja kwenye vikao hivyo kumesababisha baadhi ya majimbo kuwa nyuma kimaendeleo hasa majimbo ya uchaguzi ya Pemba,licha ya ahadi walizoombea kura .
“Ni vyema Serikali kuwa na utaratibu wa kutowalipa posho ya kikao pamoja na kuwakata mishahara wajumbe ambao kazi yao ni kusinzia wakiwa barazani, kwani wamekuwa wakitafuna fedha za umma bila ya kuzifanyia kazi,” alishauri mwanasiasa huyo.
Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi katika majimbo ya uchaguzi ya Kisiwa cha Pemba wanatoka CUF kwa kushirikiana na CCM wanaunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa.
Kumekuwapo na malalamiko ya mara kwa mara katika mihimili yote miwili ya Bunge na Baraza la Wawakilishi, kwa baadhi yao kulala wakati wa vipindi vya majadiliano vikiendelea na kushindwa kuwakilisha matatizo ya wananchi wao.

No comments:

Post a Comment