TTCL

EQUITY

Tuesday, April 26, 2016

Watanzania waadhimisha miaka 52 ya Muungano

Watanzania hii leo wanaadhimisha miaka 52 ya Muungano wa TANGANYIKA na ZANZIBAR ambapo nchi hizi mbili ziliingia kwenye Mkataba wa Muungano mnamo tarehe 22 Aprili, 1964

Mkataba wa Muungano ulitiwa saini na aliyekuwa Rais wa Tanganyika, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na aliyekuwa Rais wa Zanzibar, Hayati Sheikh Abeid Amani Karume tarehe 22 Aprili, 1964 huko Zanzibar. 
Mkataba huo ulithibitishwa tarehe 26 Aprili, 1964 na mnamo tarehe 27 Aprili, 1964, viongozi wa nchi zote mbili walikutana katika ukumbi wa Karimjee, Dar es Salaam na kubadilishana hati za Muungano.
Hata hivyo hakutakuwa na sherehe za maadhimisho ya MUUNGANO kufuatia Rais Dokta JOHN MAGUFULI kuagiza fedha zilizopangwa kutumika kwa ajili ya kugharimia vinywaji, vyakula, gwaride, halaiki, burudani mbalimbali na hafla ya usiku ambazo ni zaidi ya shilingi BILIONI MBILI zitumike kupanua barabara ya MWANZA Airport katika eneo linaloanzia GHANA QUARTERS hadi uwanja wa ndege wa MWANZA.
Barabara hiyo inafanyiwa upanuzi kutatua msongamano mkubwa wa magari ambao umekuwa ukiathiri shughuli mbalimbali katika eneo hilo.
Wananchi wametakiwa kuadhimisha sherehe hii wakiwa majumbani au wakiwa katika shughuli zao binafsi.

No comments:

Post a Comment