TTCL

EQUITY

Tuesday, April 26, 2016

Chama cha FREEDOM PARTY chashinda duru ya kwanza ya urais


Matokeo ya awali yanaonyesha kiongozi wa chama hicho NOBERT HOFER ameshinda kwa asilimia 36.7 ya kura.
Matokeo hayo yana maana kuwa kwa  mara ya kwanza tangu mwaka 1945, AUSTRIA haitakuwa na Rais anayetokea chama cha Social Democrats wala chama cha People's Party.
Wagombea wawili walioteuliwa na vyama tawala walishindwa kufuzu katika duru ya pili ya uchaguzi inayotarajiwa kufanyika tarehe 22 mwezi ujao.
Ushindi huo wa chama cha FPO unadhihirisha kutoridhishwa kwa wapiga kura na hali ilivyo katika kuendeshwa kwa masuala ya AUSTRIA.

No comments:

Post a Comment