TTCL

EQUITY

Tuesday, April 26, 2016

Afrika inaweza kuwa haina malaria ifikapo 2020

Mataifa sita ya Afrika yanaweza kuwa salama na Malaria hadi ifikapo mwaka 2020, kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la afya duniani iliyotolewa jana mjini Geneva kuadhimisha siku ya Malaria ulimwenguni .
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani -WHO - Dokta Margaret Chan.
Mojawapo ya malengo ya shirika la WHO kwa mradi wa kupambana na Malaria kati ya mwaka 2016 hadi 2030 ni kuteketeza homa ya Malaria katika nchi angalao 10 hadi mwishoni mwa mwaka 2020.
"Shirika la WHO linakadiria mataifa 21 yanaweza kulifikia lengo hilo,ikiwa ni pamoja na mataifa sita ya eneo ambako mzigo wa maradhi hayo ni mzito zaidi-limesema shirika hilo lenye makao yake makuu mjini Geneva.

Nchi hizo sita ni pamoja na Algeria,Botswana,Cape Verde,Comoros,Afrika Kusini na Swaziland. Mataifa mengine yanayoaminiwa yanaweza kuangamiza Malaria hadi mwisho wa mwaka 2020 ni pamoja na China Malaysia,Korea ya kusini,Saud Arabia,Oman,Srilanka,Timor Mashariki ,Nepal,Bhutan na mataifa manane ya Latin Amerika. Kwa mujibu wa ripoti ya WHO,watu 214 milioni wanaugua homa ya Malaria iliyoangamiza maisha ya watu 438.000.
Asili mia 90 ya waliokufa ni kutoka eneo la Afrika kusini mwa jangwa la Sahara.

No comments:

Post a Comment