TTCL

EQUITY

Tuesday, April 26, 2016

Matokeo ya awali ya uchaguzi SERBIA yaonesha VUCIC anaongoza

 
ALEKSANDAR VUCIC
Matokeo ya awali ya uchaguzi uliofanyika jana nchini SERBIA yanaonesha kuwa Waziri mkuu  ALEKSANDAR VUCIC ameshinda  baada Chama chake cha  Progressive Party kuongoza kwa kupata asilimia 57 ya kura zilizopigwa.
VUCIC ambaye amekuwa waziri mkuu wa SERBIA tangu mwaka 2014 aliitisha uchaguzi wa mapema akisema anataka kuwa na mamlaka ya kumuwezesha kufanya mageuzi yanayohitajika ili nchi hiyo iweze kuwa mwanachama wa Umoja wa Ulaya.
Kamishna wa Umoja wa Ulaya JOHANNES HAHN alikuwa miongoni mwa viongozi wa kwanza kumpongeza VUCIC kwa ushindi wake. SERBIA, taifa lenye idadi ya watu Milioni Saba lilianzisha mchakato wa kujiunga na Umoja wa Ulaya mwezi Desemba mwaka jana.

No comments:

Post a Comment