TBL Group yawapiga msasa kuhusiana na changamoto za ajira

Taasisi na makampuni mbalimbali mwishoni mwa wiki  yalishiriki katika semina ya kuwaandaa wanafunzi  wanaosoma vyuo vikuu kuingia kwenye ajira watakapomalizika masomo yao  ambayo ilifanyika katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kushirikisha wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali vya elimu ya juu.
Kampuni ya TBL Group ilishiriki katika semina hiyo ambapo Meneja wake wa kuendeleza vipaji  Lilian Makau,alitoa mada kuhusiana na jinsi ya kuhimili kufanya kazi kwenye kampuni  kubwa na zenye mifumo thabiti ya kiutendaji  na changamoto za kupata ajira.
Wanafunzi wengi pia walipata fursa ya kuuliza maswali mbalimbali kuhusu taratibu za ajira katika kampuni ya TBL ambapo aliwaeleza kuwa kampuni inatoa fursa za ajira kwa watanzania wote na taratibu zake za ajira ziko wazi na pia kuwa imekuwa na utaratibu wa kuajiri wasomi waliohitimu mafunzo vyuoni na kuwapatia mafunzo ya ndani na wengi wao wametokea kuwa na utaalamu wa kiwango cha juu baada ya muda mfupi kwenye ajira zao.

Lilian Makau
Meneja wa kuendeleza vipaji wa TBL Group, Lilian Makau akitoa mada wakati wa semina ya kuwaandaa wanafunzi wanaosoma vyuo vikuu (hawapo pichani) kuingia kwenye ajira watakapomalizika masomo yao iliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Aisec 2
Pichani juu na chini ni  baadhi ya wanafunzi wakisikiliza mada na kuuliza maswali.

Aisec 12
Aisec 7
Baadhi ya wanafunzi wakipata maelekezo kutoka kwa Meneja wa kuendeleza vipaji wa TBL Group, Lilian Makau muda mfupi baada ya kumalizika semina.