Baadhi ya walimu wastaafu mkoani Dodoma wameiomba serikali ya awamu ya tano kuharakisha malipo ya mafao yao yaliyodumu kwa miezi kadhaa sasa ili kuwapunguzia ukali wa maisha.
Wameyaeleza hayo wakati wa kipongezwa na Chama cha walimu mkoa wa Dodoma kwa utumishi wao uliotukuka ndani ya chama hicho kwa kipindi cha miaka 15.
Akikabidhi zawadi kwa wastafu hao mwenyekiti wa chama cha walimu mkoa wa Dodoma Samsoni Mkotya amesema Baraza la chama hicho taifa limendelea kutenga fedha kwa ajili ya kutoa mkono wa pongezi pindi wanachama wanapomaliza utumishi wao.
Zawadi zilizokabidhiwa kwa wastafuu hao wane ni pamoja na Bati 80 zenye thamani ya shilingi Milioni moja laki sita na elfu sitini ambapo kila mmoja amepewa bati 20.
No comments:
Post a Comment