Baada ya wilaya za Mbinga
na Songea vijijini kukumbwa na maafa ya mvua ambapo familia kadhaa
zilikosa mahali pa kuishi baada ya nyumba zao kubomoka na kuezuliwa
na mvua, maafa hayo yameikumba wilaya ya Songea mjini baada ya
nyumba ishirini kuezuliwa na kubomolewa na mvua katika mtaa wa
Ruvuma juu mjini Songea mkoani Ruvuma.
Mwenyekiti wa mtaa wa Ruvuma juu
katika manispaa ya Songea Bi. Ester Nchimbi ameeleza zaidi kuhusiana na maafa
hayo ya mvua yaliyoezua na kubomoa nyumba ishirini na kuziacha familia ishirini
zikiwa hazina mahali pa kuishi.
Kutokana na majanga hayo mbunge wa
viti maalumu wa mkoa wa Ruvuma Mheshimiwa Jackline Ngonyani Msongozi
amewatembelea waathirika wa majanga hayo na kuwapatia mabati mia moja huku
waathirika wa majanga hayo wakishukuru kwa msaada huo.
No comments:
Post a Comment