TTCL

EQUITY

Monday, January 25, 2016

Wasimamishwa kazi kwa kukiuka waraka wa serikali

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa -TAMISEMI, GEORGE SIMBA CHAWENE amewavua madaraka Mkurugenzi wa Manispaa ya DODOMA, AUGUSTINE KALINGA na Afisa Elimu Vifaa na takwimu katika manispaa hiyo JOSEPHINE AKIM kwa kushindwa kusimamia maelekezo ya serikali ya kutoa elimu bure.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa -TAMISEMI, George Simba Chawene.

Katika mkutano na waandishi wa habari mjini DODOMA, Waziri SIMBACHAWENE amesema uamuzi huo umefuatia viongozi hao kuandika waraka unaoelekeza wakuu wa shule katika Manispaa hiyo kuchangisha fedha kutoka kwa wanafunzi.

Amesema Afisa Elimu Msingi wa Manispaa hiyo SCHOLA KAPINGA amepewa onyo kali kwa kuanza kutekeleza waraka huo unaopingana na maelekezo ya Rais JOHN MAGUFULI.

No comments:

Post a Comment