KESI ya kupinga bomoabomoa iliyotarajiwa
kutolewa maamuzi leo jijini Dar es Salaam katika Mahakama Kuu kitengo
cha ardhi imeahirishwa tena, badala yake hukumu itatolewa Januari 26, 2016 siku ya jumanne .
Kesi hiyo ilifunguliwa na Mbunge wa
Kinondoni, Maulid Mtulya, (CUF) ambayo inataka wananchi hao mbali na
kubomolewa wapewe maeneo mbadala na yenye usalama ambapo wakili wa
upande wa mlalamikaji akiwa ni Abubakar Salim aliyewataka wananchi
waliokuwa nje ya mahakama hiyo kutochoka kuendelea kufuatilia kesi hiyo.
Mahakama
Kuu Kitengo cha Ardhi jijini DAR ES SALAAM imeahirisha kesi ya kupinga
ubomoaji wa nyumba za wakazi 681 wa kata tatu za Halmashauri ya Manispaa
ya KINONDONI zinazodaiwa kujengwa katika maeneo oevu na ya wazi
Mahakama Kuu Kitengo cha Ardhi jijini DAR ES SALAAM
imeahirisha kesi ya kupinga ubomoaji wa nyumba za wakazi 681 wa kata
tatu za Halmashauri ya Manispaa ya KINONDONI zinazodaiwa kujengwa katika
maeneo oevu na ya wazi.
wakili anayewawakilisha wakazi hao Abubakar Salim.
wakili anayewawakilisha wakazi hao Abubakar Salim.
Akizungumza nje ya jengo la Mahakama ya Ardhi, wakili
anayewawakilisha wakazi hao ABUBAKAR SALIM amesema uamuzi huo umefikiwa
na jaji PANTERINE KENTE kutokana na kutokamilika kwa baadhi ya vielelezo
juu ya kesi hiyo.
Aidha wakili SALIM amewataka wakazi hao kuwa watulivu wakati wakisubiri uamuzi wa mahakama.
Zoezi la bomoa bomoa limeendelea kufanyika maeneo mbalimbali hapa
nchini kwa kubomoa nyumba zilizojengwa maeneo oevu, ya wazi na
mabondeni.
Wakili wa mlalamikaji anayesikiliza kesi hiyo, Abubakar Salim,
akihojiwa na wanahabari baada ya kutoa taarifa kwa wakazi waliobomolewa
nyumba zao mabondeni waliokuwa wamejitokeza kusikiliza kesi ambayo
maamuzi yake yatatolewa jumanne 26 januari 2016.
Baadhi ya wananchi waliofika mahakamani hapo wakimsikiliza wakili Salim (hayuko pichani).
No comments:
Post a Comment