Serikali imetoa wiki mbili kwa baraza
la taifa la hifadhi na usimamizi wa mazingira nchini kuchukua sampuli
za maji yanayotiririka kutoka mgodi wa North Mara na kutoa hadharani
matokeo uchunguzi wake ikiwa njia moja wapo ya kumaliza kabisa kilio cha
miaka zaidi ya kumi kuhusu madai ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka
mgodi huo kuwa maji hayo yamekuwa yakisabisha madhara makubwa kwa
binadamu vikiwemo vifo vya watu, mifugo na kuathiri vyanzo vya maji
katika maeneo hayo.
Naibu waziri wa nchi, ofisi ya makamu wa rais, muungano na
mazingiraMh Luhaga Mpina, ametoa agizo hilo baada ya kutembelea maeneo
yote ya mgodi wa North Mara ikiwa pamoja na kukagua mabwawa
makubwayanayotumika kuhifadhi mabaki ya maji kutoka mgodi huo kasha
kuzungumza na uongozi wa mgodi pamoja na viongozi mbalimbali ngazi ya
wilaya, kata na vijiji kumi moja vinazunguka mgodihuo.
Katika taarifa yake kwa naibu waziri huyo wa nchi, ofisi ya makamu
wa rais, muungango na mazingira, meneja mkuu wa mgodi huo Bw Gary
Chapman, amesema pamoja na madai hayo ya wananchi lakini mgodi wake ni
miongoni mwa migodi nchini unaozingatia kwa kiasi kikubwa uhifadhi wa
mazingira hata kufikia hatua ya kupewa tuzo mbalimbali za kutoka mamlaka
zinazojihusisha na uhifadhi wa mazingira.
Naye mkuu wa wilaya ya Tarime Bw Groriuosluoga, akizungumza mbele
ya viongozi hao wa vijiji vinavyozunguka mgodi huo, amemuomba kiongozi
huyo kufikisha malalamiko ya fidia za nyumba zawananchi katika wizara ya
nishati na madini ikiwa utekelezaji wa ahadi ya rais John Pombe
Magufuli katika kumaliza kabisa migogoro ya mara kwa mara inayotokea
katika eneo hilo.
No comments:
Post a Comment