Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo Zitto Zuberi Kabwe
Katika
taarifa yao waliyoitoa kwa vyombo vya habari jana Jijini Dar es salaam
umoja huo umesema kuwa kiasi hicho cha fedha kilichotengwa ni kidogo
kisichoweza kukidhi mahitaji muhimu ya upatikanaji wa elimu bora nchini.
Ngome hiyo ya Vijana wa ACT Wameitaka serikali iongeze kiasi cha
ruzuku ili kukidhi dhana ya elimu bure na mahitaji ya shule hadi kufikia
sh.elfu 40 kwa kila mwanafunzi wa sekondari na sh. elfu 25 kwa mwaka
kwa mwanafunzi wa shule ya msingi.
Aidha katika taarifa yao hiyo vijana hao wameziomba kamati za shule
za wazazi kufuatilia kwa karibu fedha hizo za ruzuku na matumizi yake
kwa shule husika ili kuepuka ubadhilifu wa aina yoyote.
No comments:
Post a Comment