TTCL

EQUITY

Thursday, December 24, 2015

Mtu mmoja aliyejifanya Afisa wa mamlaka ya mapato TRA atuhumiwa kwa utapeli.

Mtu mmoja ambaye hakufahamika jina lake mara moja aliejifanya Afisawa mamlaka ya mapato - TRA aliyekuwa na gari lenye namba za usajili T945  BYG amenusurika kifo mara baada ya kula kichapo kutoka kwa wananchi wakati akiwa kwenye harakati za kufanya utapeli kwenye duka kubwa la VEW POINT lililopo Tabata Segerea jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa wafanyakazi wa duka hilo mtu huyo aliejifanya afisa kutoka mamlaka ya mapato TRA sio mara ya kwanza kufika eneo hilo kwani siku moja kabla  alifika akiwa na wenzake wawili na mmoja waliyemtambulisha kuwa ni mwandishi wa habari  na kufanikiwa kutapeli kiasi cha shilingi milioni tano.
 
Mtuhumiwa huyo sasa  amekamatwa na  kufikishwa kituo cha polisi Tabata Segerea kwa hatua zaidi za Kisheria.

No comments:

Post a Comment