TTCL
EQUITY
Thursday, April 2, 2015
KIKAO CHA BARAZA LA MADIWA ARUSHA CHAVUNJIKA
kikao cha baraza la madiwani kimevunjika leo na kuahirishwa hadi week
ijayo. Sababu iliyopelekea hali hiyo ni hatua ya
madiwani chadema kutoa hoja ya kutojadiliwa
kabrasha hadi hapo hoja zake mbili
zitakapojadiliwa. Hoja
za Nanyaro ambazo
ziliungwa mkono na madiwani wenzake wa
CHADEMA ni:
1:Vifaa vya zaidi ya 500mil vilivyoibwa na
aliyekuwa daktari wa jiji virejeshwe na mwizi
akamatwe.
2:database ya mapato
Alisema swala la vifaa vya Levolosi na Data
base ya zaidi ya miaka miitatu amekuwa
akitaka hatua zichukuliwe ila hadi sasa hakuna
chochote badala yake mkurugenzi wa jiji
amekuwa sehemu ya
tatizo. Kwa
msisitizo
akasema, taarifa za baraza yaani kabrasha limejaa
uongo na halifai
kujadiliwa.
Baada
ya hoja hiyo
diwani Doita aliunga mkono kisha kufuatiwa na
madiwani wote wa CHADEMA hali ambayo ilimlazimu
mwenyekiti wa kikao kuahirisha kikao kwa
muda.
Baada ya muda madiwani wote wa CHADEMA wakipaza sauti zao kwa umoja wao
walisisitiza kutokuendelea na kikao hadi hapo
nidhamu na uwajibikaji wa mkurugenzi na
watu wake kwa manufaa ya wananchi wa
Arusha
Msimamo wa CHADEMA hasa kwenye swala la
mapato ya jiji ni kuwa Jiji lina uwezo wa
kukusanya zaidi ya mapato ya sasa licha ya
mafanikio makubwa ya makusanyo ya
1.2 Bil
kwa mwezi kutoka
400 mil
awali. Pia
makusanyo
haya yawe kwa njia ya electronic.
No comments:
Post a Comment
Newer Post
Older Post
Home
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment