TTCL

EQUITY

Saturday, January 4, 2014

Nini siri ya mafanikio kwenye uhusiano?

  black couple in bed 1
1-Usijisahau na hakikisha unarudisha uliyokuwa ukimfanyia mwenza wako miaka 4 iliyopita, kabla hamjafunga ndoa, yafanye tena sasa. Inawezekana
maisha yenu yamebadilika na sasa mmekuwa familia kwamba kuna watoto,
bado watoto hawakuzuii wewe mume/mke/mpenzi kuwa wapenzi. Ndio ni
baba na mama lakini pia ni Wapenzi.

2-Jipende ili uvutie, usipojipenda wewe mwenyewe na kuvutia itakuwa ngumu kwa
mwenzio kuvutiwa nawe. Kwavile tu mmefunga ndoa au mnaishi pamoja
haina maana ndio mwisho wa kuvutia.

3-Penda/pendezwa,
kukubaliana au kubali mchango wa mawazo yake kwenye jambo mnalotaka
kufanya, mshirikishe mwenza wako kabla ya kufanya uamuzi wowote,
peaneni matumaini na ushirikiano inapobidi....sio kila wakati wewe
ndio msemaji mkuu na muamuzi wa mwisho na yeye ni wa kupokea tu, hata
akichangia mawazo yake huyafanyii kazi(unadharau).

4-Muda, kazi na watoto huchukua muda mwingi na hivyo kutopata muda wa
kuzungumza na kuonyeshana mapenzi, hivyo kutenga muda wenu kama
wapenzi ni muhimu. Ninaposema muda wenu kama wapenzi sina maana ya
kufanya ngono kwani ngono inaweza kufanyika watoto wakiwa wamelala,
nazungumzia ule muda wa ninyi wawili kama ilivyokuwa mf: miaka 4
iliyopita kabala hamjafunga ndoa.

5-Mawasiliano kwa maana ya kuzungumza ni njia pekee ya kumwambia mwenza wako vile unavyojisikia, unataka nini, kwanini umefanya jambo fulani, usaidiwe
vipi, kwanini uko hivyo ulivyo n.k. Hii ni njia pekee ya kuwekana sawa na kuepuka maumivu ya kihisia ambayo yanaweza kukupa upweke ndani ya uhusiano/ndoa.

6-Kubali mabadiliko,
jinsi miaka inavyozidi kusonga ndivyo ambavyo tunabadilika/tunakua,
maisha yetu yanabadilika....japokuwa wakati mwingine mabadiliko hayo
hayaji kama tulivyotarajia bado hatuna budi kuyakubali na kwa pamoja
ku-adopt badala ya kulalamika na kufananisha.

7-Kuzozana/gombana kwa maneno, kubishana sio ukorofi inategemea mnabishanaje na kuhusu nini? Katika hali halisi kubishana kwenye uhusiano kunahashiria afya ya uhusiano wenu....ikiwa kuna watu wanaishi pamoja kama wapenzi na hawajawahi kubishana basi ni either wanadanganya au mmoja wao anamuogopa mwenzie.

Pamoja na kuwa ninyi ni wapenzi bado mnatofautiana kijinsia, kimawazo,
kikazi, kipato, matumzi binafsi ya pesa, kimalezi na hata kasoro zenu
hazifanani....hivyo kubishana ni lazima ikiwa kunatofauti hizo na
nyingine ambazo unazijua.

Kubishana kunaweza kuwasaidia mmoja wenu kujirekebisha kwani itawawezesha
kutambua kosa lako ni lipi hasa kama mwenza wako sio mtu wa kukosoa
papo kwa hapo (kosa linapotokea), pia itakuwa nafasi nzuri ya kutambua au kugundua nini hasa mwenzako anafikiria kuhusu kosa/tendo ulilofanya au tabia yako na nini anataka kifanyike ili kuepuka mabishano ya mara kwa mara.

8-Shukuru, omba radhi ni maneno mafupi na pengine unaweza kudhani kuwa hayana umuhimu wowote, licha ya kwamba yanaashiria kuwa umelelewa katika maadili mema pia yanauzito na maana kubwa sana kwenye maisha yetu kuliko unavyofikiria.

Unapohisi kuwa umemuudhi mwenza wako, sio mpaka akununie kwa wiki moja au
akufokee ndio uombe radhi, akionyesha tu kuwa hajafurahia tendo lako
au maneno yako basi omba radhi.

Shukuru kwa kila jambo unalofanyiwa na mpenzi wako....unakumbuka wakati
mnaanza uhusiano akiku-check during the day unasema “asante mpenzi
kwa kunijulia hali”, sasa kwanini ushindwe kusema asante kwa chakula mpenzi?!!

No comments:

Post a Comment