TTCL

EQUITY

Saturday, January 4, 2014

Maisha ya Kitandani...!

black-couple-in-bed
Leo nitagusia kidogo tu namna ya kubadili mwenendo wa Maisha yako ya Kingono ili kufurahia zaidi uhusiano wako wa kimapenzi na mwenza wako. Najua unatambua kuwa kwenye kila uhusiano wa kimapenzi kuna “maisha ya kimapenzi” na “Maisha ya kingono”

Kitu cha kwanza unachopaswa kuzingatia ni kutambua na kukubali kuwa kuna vitu ambavyo huwezi kuvibadilisha na hivyo basi unatakiwa kujifunza kuishi navyo kwa kuvichukulia kama vilivyo, kuvidharau au kutafuta namna ya kuvifurahia.

Kwenye kubadilisha mwenendo wako wa kingono unategemeana zaidi na wewe mwenyewe au ninyi wenyewe kama wenza kwani routine huwa zinatofautiana na vilevile hubadilika kutokana namazingira, mtindo wa maisha yenu .

Kuna ile “routine” ya kushikana-shikana mikono ikiwa mikavu tena kwa kuanzia mapajai kupanda juu, badilisha hiyo na sasa tumia mafuta ya ngozi ya maji yasiyo na harufu (baby oil inafaa) au lotion mnayotumia kwa ajili ya ngozi kuepuka matatizo ya ngozi na badala ya kuanza kushikana mapajani kwenda juu anzia popote alafu bila kufuata "routine". Hilo moja.

Pili, sote tunajua uhusiano mkubwa uliopo kati ya vyakula tunavyokula na uzuri wa miili na ngozi zetu, pia niliwahi kuelezea uhusiano wa ngono na ngozi, mwili wa kuvutia na wepesi wakati wa kufanya ngono! Basi badili mtindo wako wako wa kula ili ngozi na mwili wako upendeze na kuvutia na hivyo kuwa managable kitandani (wakati wa kufanya mapenzi).

Tatu, Ondoa shombo ya Uke wako kwa kujiswafi angalau mara mbili kwa siku, ikiwa harufu ya Utoko haiishi pamoja na jitihada zako za kujiswafi basi kupunguza au acha kabisa kunywa Pombe, ukiweza ongeza ulaji wa maziwa ya Mgando (mtindi) asilia, matunda na mboga mboga bila kusahau unywaji wa maji badala ya vinywaji ambavyo vina sukari nyingi (soda). Unapokuwa na Uke msafi,inakuongezea hali ya kujiamini na hivyo kufurahia na kujiachia kwa mpenzi wako bila kuweka mipaka au kujishitukia/ kujishuku kuwa unatoa kijiharufu.

Nne, Jifunze kuizungumzia ngono na mpenzi/mwenza/mumeo kwa njia za kisasa za kimawasiliano, Mf: kumwambia kilichofanyika jana usiku na nini hasa kilikupendeza, unachotarajia kumfanya usiku wa leo, nini ungependa kufanyiwa/kujaribu. Usipo ongea na mpenzi wako katika mtindo wa kingono-ngono au kimahaba kwa njia za kisasa za kimawasiliano alafu ikatokea Mf:“facebook friend” au BBM contact akawa anazungumzia hayo kwa mke/mume basi usije kushangaa kuona mwenza wako anatumia muda mwingi kwenye BBM, Facebook au mikusanyiko mingine ya Mtandaoni (wapo wakaka na wadada wanapenda sana mtindo huu wa kuongea na wapenzi wa watu wenyewe wanaita ku-flirt).

Hakuna mtu asiependa ku-flirt lakini unapokuwa kwenye uhusiano/ndoa unaweza kudhani kuwa huitaji kufanya hivyo tena, kiukweli unaweza kabisa ku-flirt na mwenza wako na ninapenda kukuhakikishia kutokana na uzoefu wangu kuwa "mtindo huo wa mawasiliano" huwaongezea chachu kwenye uhisiano wenu na ile hamu ya kutaka kuwa pamoja japokuwa mnaishi pamoja. Yaani unatamani kurudi
nyumbani kuwa na mume/mke wako kuliko kukaa Bar au Salon.

Tano, ongeza kiwango cha "romance" kwa kuwa na mazoea ya kubadilishana mate au kubusu shingo na kuitafuna kimahaba, kunyonya chuchu bila kukusudia kufanya ngono, kwamba unafanya hivyo kama sehemu ya kuonyesha mapenzi au ukaribu wenu kama wapenzi.....sio msubiri mpaka mnapokwenda kufanya mapenzi. Jitahidi kutumia midomo na ulimi mara kwa mara mnapokuwa pamoja.

Sita, jifunze Kuponografika ikiwa mwenzio anapenda hizo bue movies, karibu wanaume wote wanazipenda hizi kitu na sio dhambi kuziangalia kwa pamoja kama mnaweza ila tu angalieni msipitilize na kuwa addicted. Natambua huwezi kujifunza jambo lolote ili kuboresha uhusiano wako lakini unaweza kuburudika kama anavyoburudika yeye (mimi Binafsi sipendi kuona watu wanangonoka).

Saba, Kuza au ongeza uwezo wako wa kungonoka kwa kujitahidi kufanya ngono mara kwa mara, jinsi unavyofanya mara nyingi kwa mitindo na mikao tofauti ndivyo ambavyo utakuwa na hamu ya kutaka kufanya tena...unajua zile “moments” za kila “event” ndizo zitakazokuongezea nyege kila utakapokuwa unazikumbuka na hivyo kumtamani mwenza wako na kutaka kufanya tena na tena.....

No comments:

Post a Comment