TTCL

EQUITY

Saturday, January 4, 2014

Jifunze kuwa mbunifu

How not to foster creativity: A cartoon on the creative process by Mr. Fish (Source: Truthdig.)
Makala hii inachambua kwa kifupi jinsi ya kuwa mbunifu. Haijalishi ubunifu ni wa namna gani - iwe kuandika kitabu, kuzalisha vyakula, kutoa huduma za ufundi n.k , yote hayo yanaweza kufanyika kwa ubunifu na kuleta manufaa.
Zingatia hatua zifuatazo:-
 
1. Jifunze kulikubali tatizo kama changamoto na fursa ya kuleta suluhisho: Wapo wengi ambao wanapoona ugumu katika jambo fulani, wanasita kuendelea au wanasubiri suluhisho toka kwa wengine. Ni kweli kuna mambo utawaachia wengine, lakini lile 'lililo karibu' na uwezo wako waweza litatua. Mfano ukaribu ninaozungumzia hapa inawezekana ni mazingira unayoishi, aina ya ujuzi wako, na uwezo wako 
 
2. Tumia muda wa kutosha kujifunza: Ili kuwa mbunifu inakupasa uwe na taarifa za kutosha kuhusu tatizo unalotaka kutatua, ujue pia wengine wamefanya nini. Kujifunza ndio kunakopelekea uzoefu, na uzoefu au kubobea katika kitu ndiko kunakoleta ubunifu. Kumbuka kujifunza sio lazima uende darasani, waweza jifunza kwa kuona, kusikia, kujisomea, au kwa kufundishwa-darasani au sehemu nyingine yoyote ile.
"Ubunifu ni namna tuu ya kuunganisha vitu. Ukiwauliza watu wabunifu waliwezaje kufikia walivyofanya, wanajisikia hatia kwakuwa kiukweli hawakufanya lolote, bali waliona tuu kitu fulani. Ilionekana wazi kwao baada ya muda fulani. Hiyo ni kwa sababu waliweza kuunganisha uzoefu waliokuwa nao, na kuweka vitu kwa pamoja.Na sababu ya wao kuweza kufanya hivyo ni kuwa walikuwa na uzoefu, au walitumia muda mwingi zaidi kufikiria kuliko watu wengine, kuhusu uzoefu wao".

3. Thubutu Kuota: Baada ya kulitambua tatizo, ukawa tayari kulitatu, ukajawa na hamasa ya kujifunza, na ukajifunza vya kutosha kuhusu hali husika, kinachofuata ni wewe sasa kufikiria suluhu ya tatizo husika. Unachopasa sasa ni kupendekeza njia tofauti ya kufanya jambo, aina mpya ya bidhaa au huduma, na kujaribu hicho unachofikiria ili kilete mafanikio. Katika hali hii, Usiogope kukosea, na wala usiogope kuwa kitu chako kitakataliwa au kuonekana cha ajabu mbele ya watu wengine. Kwani kiuhalisi, ni kweli ni kitu tofauti hivyo jinsi watu wengine watakavyokipokea itakuwa tofauti.
Kuwa mbunifu sasa..!!!

No comments:

Post a Comment