Kuna jamaa mmoja kwa muda mrefu alikuwa na mke mdogo kwa siri katika
jiji la ...... Siku moja katika kutenga muda wa kutosha wa kujirusha na
bi mdogo jamaa kapanga safari ya kikazi na kumuaga mke wake kuwa
anakwenda Arusha kikazi wiki nzima. Kumbe huku nyuma alipanga kutanua na bi
mdogo.
Baada ya starehe za usiku wa jana yake na bi mdogo huyo, jamaa akiwa ofisini aliamua kumtumia ujumbe wa simu nakushukuru bi mdogo
Jamaa katuma ujumbe huu;
“Asante baby kwa staili ya jana, ilikuwa kali sana na nimeipenda. Ndio
maana nakupenda wewe kuliko wanawake wote duniani” >>>> na kuituma.
Baada ya kutuma jamaa kagundua kakosea namba na ilienda kwa waifu, yaani kwa mke wa ndoa
Jamaa katika kuhaha kuzuia ujumbe usimfikie mke wake alikwenda kwa
wahudumu wa mtandao wa simu ili kuomba msaada wa kuzuia meseji na mazungumzo
yakawa hivi:
Jamaa: Kuna meseji nilikuwa niitume kwa bi mdogo kwa bahati mbaya imekwenda kwa waifu wangu, je mnaweza kuizuia?
Mhudumu: Wahi fasta kwenye mnara ukaizuie....
No comments:
Post a Comment