TTCL

EQUITY

Saturday, August 24, 2013

Ombi la Kimemia kutaka atoe ushahidi faraghani lakataliwa

Francis Kimemia
Bw Francis Kimemia (kushoto) akiwa kortin

OMBI la katibu wa Baraza la Mawaziri Francis Kimemia kutaka atoe ushahidi faraghani dhidi ya mwanablogu aliyedai mtumishi huyo mkuu wa umma alifanya mkutano wa siri Alhamisi lilikataliwa na mahakama.
Bw Kimemia alilazimika kutoa ushahidi wake mahakamani baada ya mshtakiwa Robert Alai kupinga ombi hilo la kufanyiwa kesi faraghani akisema “hakuna sheria inayoruhusu hayo akiongeza afisa huyo mkuu wa serikali sio maalum ili akubaliwe kutoa ushahidi kwa siri.”
Hakimu mwandamizi Joseph Karanja wa Mahakama ya Milimani Nairobi alikataa ombi hilo la Bw Kimemia, mwenyekiti wa tume huru ya uchaguzi na mipaka (IEBC) Isaac Hassan
Bw Kimemia aliamriwa afike kortini kutoa ushahidi katika kesi inayomkabili Bw Alai ya kuchapisha habari katika mtandao kwamba katibu huyo alikuwa anakutana na Jaji Isaac Lenaola, mwenyekiti wa IEBC Ahmed Isaack Hassan na aliyekuwa wakati mmoja mkuu wa polisi Meja Jenerali Mstaafu Mohammed Hussein Ali.
Bw Kimemia alidaiwa alikuwa anajaribu kuwashawishi kuhusu kesi ya kupinga uchaguzi wa Rais Uhuru Kenyatta na Bw Raila Odinga iliyokuwa inasikizwa katika Mahakama ya Juu.
“Sijawahi kutana na watu hao wanaodaiwa nilikutana nao na kamwe sijawahi kukutana na Alai,” alisema Bw Kimemia.
Bw Alai ameshtakiwa kwa kutuma ujumbe wa kuudhi.
Alhamisi wakili anayemtetea Bw Alai alimtaka Bw Kimemia awasilishe thibitisho kwamba ni yeye alichapisha ujumbe huo katika mtandao.
Katibu huyo alisema maafisa wanaochunguza kesi hiyo wanajua jinsi walimuhusisha Bw Alai na taarifa hizo.
“Nilifahamishwa na marafiki kwamba kulikuwa na taarifa katika mtandao kwamba nilikutana na Jaji Lenaola, mwenyekiti wa IEBC Bw Ahmed Isaack Hassan na aliyekuwa Kamishna wa Polisi Meja generali (mstaafu) Ali Mohammed,” alisema Bw Kimemia.

Kuapishwa
Alisema wakati taarifa hizo zilikuwa zinachapishwa alikuwa mwenyekiti wa kamati andalizi  ya sherehe za kuapishwa kwa rais mpya na kwamba watu wengi walikuwa wanasoma taarifa alizotuma Alai.
“Hakukuwa na ukweli wowote kwamba nilikuwa nakutana na watu hao katika kilabu cha Karen Blixen,” Bw Kimemia alimweleza Bw Karanja na kuongeza "sijui nilikuwa wapi siku niliyofahamishwa kuhusu ujumbe huo uliotumwa katika mtandao.”
Alisema hakuwapigia watumishi wenzake simu kwa vile “taarifa hizo zilikuwa za uwongo.”
“Kama afisa mkuu wa serikali taarifa hizo zilinikera na kuniahibisha mbali na kudai kwamba sifai kuhudumu katika wadhifa wangu,” alisema.
Alisema alimpigia simu Mkurugenzi wa CID Ndegwa Muhoro achunguze taarifa hizo.
Bw Kimemia alisema punde tu kesi hiyo itakapokamilika atamshtaki Bw Alai kwa kumharibia jina.
Kesi hiyo iliahirishwa hadi Septemba 6.

No comments:

Post a Comment