TTCL

EQUITY

Wednesday, December 9, 2015

Viongozi wa serikali na wananchi wajitokeza kwa wingi katika maeneo mbalimbali kutekeleza agizo la rais Kufanya Usafi


Rais John Magufuli ameagiza siku ya Uhuru itumiwe kufanya usafi
Rais John Magufuli ameongoza kwa vitendo zoezi la kufanya usafi leo kama alivyoelekeza baada ya kufuta shamrashamra za maadhimisho ya siku ya Uhuru, Disemba 9.
Rais Magufuli na mkewe Janeth wamefanya usafi katika maeneo ya Feri, eneo ambalo liko mita kadhaa kutoka Ikulu jijini Dar es Salaam.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Samia Suluhu Hassan, aameshiriki kikamilifu  na baadhi ya wananchi wakazi wa eneo lake la Oysterbay- Karume Raod, kufanya usafi ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 54 ya Uhuru wa Tanzania kama alivyoagiza Mh. Rais Dkt. John Pombe Magufuli, ambapo zoezi hilo limefanyika nchini kote hii leo.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, Pamoja na Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Paul Makonda wakishiriki kuzoa taka na baadhi ya wananchi wa eneo Morocco, wakati wa zoezi la kufanya usafi wa mazingira ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 54 ya Uhuru wa Tanzania kama alivyoagiza Mhe Rais Dkt. John Pombe Magufuli, ambapo zoezi hilo limefanyika nchini kote hii leo.
jk2
Rais Mstaafu Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete wakifanya usafi katika soko kuu la Chalinze leo Desemba 9, 2015 ikiwa ni kuadhimisha miaka 54 ya Uhuru
Naye rais wa serikali ya awamu ya nne, Jakaya Kikwete na mkewe Salma nao wameingia barabarani na kuungana na wananchi kufanya usafi katika maeneo yao katika harakati za kutokomeza magojwa yanayotokana na uchafu kama kipindupindu.

Aidha, Makamo wa rais, Samia Suluhu yeye ameonekana akifanya usafi katika eneo la ufukwe wa bahari wa ‘Coco Beach’ jijini Dar es Salaam huku Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa yeye ameingia katika eneo la Soko la Kariakoo kujiunga na zoezi hilo.

Wananchi wa Mkoa wa Dodoma wakitekeleza agizo la Mh. Rais Maguful, la kufanya ufafi
Wananchi kwa ujumla nchini wameonekana kuitikia wito wa kufanya usafi katika maeneo yao kwa hamasa kubwa hali inayoonesha kuwa Tanzania itaweza kutokomeza magonjwa ya mlipuko yanayotokana na uchafu.
Wananchi wa Jimbo la hai Mkoani kilimanjaro wakishirikiana na Mh. Mbunge Freman Mbowe katika zoezi la kufanya usafi
Baadhi ya wasichan warembo wakishiriki kuunga mkono agizo la Rais kwakufanya usafi katika Jiji la Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment