Ukumbi wa Julius Nyerere mjini Dar es Salaam |
15.38pm:Waandishi wa habari
wajiandaa tayari kwa matokeo ya uchaguzi mkuu katika ukumbi wa mikutano
wa Julius Nyerere mjini Dar es Salaam.
17.16pm:Muungano wa upinzani nchini Tanzania UKAWA umedai kwamba vijana wake 200 ambao walikuwa wakikagua matokeo yanayotolewa kutoka kwa maajenti wake katika vituo vya kupiga kura kote nchini walikamatwa usiku uliopita na sasa wako kizuizini.
Naibu mwenyekiti wa muungano huo Profesa Abdalla Safari amesema kuwa vijana hao walikamatwa wakati maafisa wa polisi walipovamia vituo vya uchaguzi vya upinzani na kuchukua data muhimu na kompyuta.
Muungano huo umedai kwamba hatua hiyo ya maafisa wa polisi itawalazimu kupinga matokeo yoyote yatakayotolewa na tume ya uchaguzi NEC, ukisema kuwa umewachwa bila ushahidi wa kuonyesha kwamba kuna udanganyifu katika matokeo ya uchaguzi.
Umesema kuwa hautakubali matokeo hayo huku profesa Simba akisema kuwa uwezo wa raia utaamua mwelekeo wa taifa iwapo matokeo hayo hayatawapendelea.
Maelekezo kwa lugha mbili.kichina na kiingereza katika jumba la mikutano la Julius Neyerere jijini Dar es Salaam |
14.25pm:Maelekezo katika jumba la mikutano la Julius Nyerere mjini Dar es Salaam yameandikwa kwa lugha mbili,kichina na kizungu.toa maoni yako
Njia iliofungwa kisiwani Zanzibar |
Ukumbi wa matokeo ya uchaguzi kisiwani Zanzibar |
13.16pm:Upigaji kura unaendelea katika vituo vyengine 42 kati ya zaidi ya vituo 60,000 baada ya kushindwa kupiga kura siku ya jumapili kutokana na matatizo tofauti.
Maafisa wa polisi |
Moody Awori kiongozi wa ujumbe wa waangalizi Afrika mashariki |
10.56am:Kuna hali ya wasiwasi mjini Mwanza huku maafisa wa polisi wakikabiliana na vijana wanaodaiwa kutoka katika chama cha UKAWA. Kuna visa ambapo vikosi vya usalama vilirusha gesi za kutoa machozi ili kuwatawanya waandamanaji.
Mwanza |
Julius Nyerere |
Maafisa wa usalama huko Mwanza |
Vijana wailalamikia tume ya uchaguzi |
9.28am: Wazee na walemavu ndio watu walioathirika zaidi na tataizo hilo kwa kuwa iliwabidi wangojee tena.Hatahivyo wamewasili katika kituo hicho.
Masanduku ya kupigia kura |
Tume ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania imesema itaendelea kutoa matokeo ya uchaguzi wa urais leo kutokana na yanavyo wafikia. Hata hivyo kuna maeneo ambayo uchaguzi haukufanyika Jumapili hivyo yamefanyika leo hii, na bado zoezi la kuhesabu linaendelea na baadae kupeleka majumuisho katika majimbo yao ilikutumwa katika tume ya uchaguzi Dar es salaam.
Bonyeza hapa kwa habari za karibu zaidi kuhusu matokeo ya kura
No comments:
Post a Comment