TTCL

EQUITY

Wednesday, June 26, 2013

UJIO WA OBAMA AFRIKA

Obama anaanza ziara yake

Rais Barack Obama anaanza ziara yake ya pili rasmi barani Afrika kama rais wa Marekani (26.06.2013). Ataanzia ziara hiyo nchini Senegal, kabla ya kwenda Afrika Kusini na kumalizia Tanzania.
Maratajio yalikuwa makubwa barani humo alipochaguliwa rais huyo mwenye asili ya kiafrika kuwa rais mwaka 2008. Nani kama si yeye ambae angetoa kipaumbele kwa bara la Afrika? Mhula wake wa pili ulipoanza matarajio hayo kidogo yamepwaya.Juhudi zake kuwelekea Afrika zinaonyesha hafifu zikilinganishwa na zile za mtanagulizi wake.
"Nna daamu ya kiafrika mwilini mwangu na historia ya familia yangu mwenyewe inachanganya tangu misiba mpaka mafanikio ya historia ya bara la Afrika." Hayo ndiyo matamshi aliyochagua kuyatamka rais Barack Obama aliefanya ziara fupi nchini Ghana mwaka 2009.

US President Barack Obama (2nd R), First Lady Michelle Obama (5th, L), their daughters Sasha (3rd R) and Malia (3th L) stand at the entrance of the 'Door of No Return' during a guided tour in Cape Coast Castle, a former slavery outpost, in Cape Coast, Ghana, on July 11, 2009. The visit marks Obama's first to subsaharan Africa as president. AFP PHOTO / Saul LOEB (Photo credit should read SAUL LOEB/AFP/Getty Images) 
Rais Obama na familia yake walipokaribishwa Ghana 11-07-2009

Furaha na shangwe zilikuwa kubwa alipotaja asili yake ya kiafrika. Kwamba wakati huo huo alilaani rushwa barani Afrika na kushinikiza watu wawajibike, hayo watu waliyafumbia masikio. Nani kama si rais wa kwanza wa Marekani mwenye asili ya kiafrika, atakaefungua ukurasa mpya wa sera ya marekani kuelekea Afrika, kuhimiza vitega uchumi vya moja kwa moja na kuinua shughuli za utalii?
Hali lakini imejitokeza vyengine: Migogoro iliyoathiri sekta ya nyumba na uchumi nchini Marekani ilimlazimisha rais Obama anaesalitika zaidi na siasa ya ndani, atangulize mbele masilahi ya kijiografia na kulilenga zaidi bara la Asia na wakati huo huo kuelekeza mawazo yake katika bara la Afrika.

Kauli za wasomi kuhusu ziara hiyo
Professor David Shinn aliyewahi kuwa balozi wa Marekani nchini Ethiopia na Burkina Faso na ambae hivi sasa ni mhadhiri wa siasa za kimataifa katika chuo kikuu cha George Washington anachambua siasa ya Marekani kuelekea Afrika kwa kusema:" Ni kweli kwamba awamu ya kwanza ya utawala wa Obama haikutoa umuhimu mkubwa sana kwa bara la Afrika. Bila ya shaka watu walijiwekea matumaini makubwa.Lakini majukumu muhimu ya siasa ya ndani yalizuka na kufanya iwe shida kushughulikia kwa nguvu masuala ya Afrika.Hilo atalisawazisha katika awamu yake hii ya pili.Ndio maana safari hii ameanza mapema safari hii ndefu".
Hata hivyo si sawa kuwasingizia Obama na wizara ya mambo ya nchi za nje ya Marekani kwamba hawajishughulishi na masuala ya Afrika. Katika mzozo wa Sudan, Obama aliingiliaa binafsi au aliwatuma wajumbe wake maalum ili kuhakikisha kura ya maoni kuhusu uhuru wa Sudan kusini inafanyika kama ilivyopangwa mwaka 2011. Mwaka uliofuatia viongozi wa Afrika walifunga safari hadi Camp David kutokana na mwaliko wa rais Obama, kuhudhuria mkutano wa kundi la mataifa manane tajiri kiviwanda uliopitisha azimio kuhusu mkakati wa kudhamini "usalama wa chakula" duniani.
Mkakati huo unaendelezwa katika nchi 20 zikiwemo Senegal na Tanzania. Hata hatua zinazozusha mabishano zimechukuliwa na serikali ya rais Obama:kwa mfano walipotuma vikosi maalum vya Marekani katika Afrika kati ili kumsaka mkuu wa waasi wa LRA Joseph Kony,au walipoanzisha ujenzi wa vituo vya ndege zinazorzushwa bila ya rubani nchini Athiopia,Niger na Djibuti.
Mwandishi:Ludger Schadomsky/Feleke,Abebe/Hamidou Oummilkheir

No comments:

Post a Comment