TTCL

EQUITY

Tuesday, February 7, 2017

'Viroba' kuhamishiwa kwenye chupa


 Image result for viroba
Serikali imesema kama sehemu ya mikakati yake ya kudhibiti unywaji wa pombe maarufu kwa jina la 'viroba' itawaagiza wafanyabiashara wanaohusika kuzihamishia pombe hizo kwenye chupa kubwa ili vijjana wanaozitumia waone aibu kuzibeba kila wakati. 

Akijibu swali la mbunge wa Kigamboni, Dkt. Fautine Ndugulile, Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage, amesema serikali ilishapiga marufuku biashara hiyo, na sasa kwa mkakati huo utasaidia kuokoa kizazi cha vijana wanaoangamia na kushindwa kufanya kazi kutokana na unywaji wa pombe hizo.
 
Mwijage amesema, pombe hizo zitakapohamishiwa kwenye chupa, gharama yake itakuwa kubwa kiasi cha kuwashinda wanafunzi kununua

Tazama Video......

No comments:

Post a Comment