TTCL

EQUITY

Wednesday, February 15, 2017

Theresa Mei kuanzisha utaratibu wa Uingereza kujiondoa katika EU

media 
Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May.REUTERS/Dylan Martinez
Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa Mei amethibitisha Alhamisi hii kwa ataanzisha rasmiutaratibu wa Uingereza kujiondoka katika Umoja wa Ulaya ifikapo mwishoni mwa mwezi Machi.
Baraza la Seneti na Bunge walipitisha Jumatano hii kwa idadi kubwa ya wajumbe nakala inayomrushu rasmi kiongozi wa serikali kutumia Ibara ya 50 ya Mkataba wa Umoja wa Ulaya ambayo itaanzisha mchakato wa Uingereza kujionda katika Umoja huo.

Kisha itabidi kuepo kwa kipindi cha miaka miwili ya mazungumzo na Umoja wa Ulaya juu ya suala la Uingereza kujiondoa katika Umoja wa Ulaya. Majadiliano yatajikita juu ya masuala ya biashara, uhamiaji na usalama.

Nakala juu ya Uingereza kujiondoa katika Umoja wa Ulaya inatazamiwa kupitishwa na baraza la Wazee wa Busara. Serikali inataka nakala hiyo ipitishwe Machi 7.

No comments:

Post a Comment