TTCL

EQUITY

Tuesday, May 3, 2016

TATIZO LA KUKATIKA UMEME NCHINI KUMALIZIKA SEPTEMBA

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo
SERIKALI inatarajia kuzindua mradi mkubwa wa kuboresha miundombinu ya kusafirisha umeme Septemba mwaka huu, utakaomaliza tatizo la umeme kukatika.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo alisema kwa sasa miundombinu ya kusafirishia umeme ni midogo na katika kuboresha hilo, kuna mradi mkubwa utazinduliwa Septemba mwaka huu wa kusafirisha umeme.
Alisema mradi huo ni wa kusafirisha umeme kutoka kilovoti 220 hadi 400 kutoka Dar es Salaam-Tanga hadi Arusha na Iringa-Dodoma-Shinyanga, hivyo tatizo la kukatika umeme litatatuliwa.
Waziri huyo alitoa maelezo hayo wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Korogwe Mjini, Mary Chatanda (CCM) aliyetaka kufahamu lini umeme utakoma kukatika wilayani Korogwe.
Akielezea hilo, Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani alisema Serikali inafanya marekebisho ya transfoma na chanzo cha umeme cha Hale mkoani Tanga ili kumaliza tatizo la kukatika umeme mara kwa mara wilayani Korogwe na mkoani Tanga kiujumla.
Akijibu swali la msingi la Chatanda aliyetaka kufahamu kama serikali haioni sasa wakati mwafaka Mji wa Korogwe na viunga vyake kuunganishwa na Gridi ya Taifa, Dk Kalemani alisema Mji wa Korogwe hupata umeme kutoka Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Hale kilichounganishwa katika Gridi ya Taifa pamoja na viunga vya mji huo pia vilivyounganishwa kwenye gridi hiyo ya taifa.
Hata hivyo, alisema mji wa Korogwe bado una maeneo ambayo hayana umeme ambayo ni vitongoji vya Bagamoyo, Habitat, Kilole Sabibo, Kitopeni, Kwadungwe, Makwei, Ruengera Relini, Ruengera Darajani na baadhi ya vitongoji vya Mtonga, Kwamkole na Kwasemangube.
Naibu Waziri alisema maeneo hayo yataingizwa katika mpango wa utekelezaji wa bajeti ya Shirika la Umeme(Tanesco) kwa mwaka wa fedha 2017/2018.

No comments:

Post a Comment