TTCL

EQUITY

Tuesday, March 1, 2016

Watumishi wa Afya watakiwa kuongeza juhudi

IMG_3605Mratibu wa shirika la Riksfobundent For Sexual Upplysning,Jonas Lillberg (kushoto) na kulia ni Jenny Fors kutoka shirika la WaterAid Sweden,wakizingua mnara wa tanki la maji katika zahanati ya kijiji cha Mwankoko manispaa ya Singida lilojengwa na SEMA kwa ufadhili kutoka WaterAid Tanzania na RFSU.
 
Watendaji  wa serikali ngazi mbali mbali ambao vituo vya afya na hospitali vimenufaika na ukarabati mkubwa wa majengo na uboreshaji wa miundo mbinu ya maji wametakiwa wafanye juhudi  za ziada kuwahamasisha  akina mama wajawazito kujifungulia kwenye vituo hivyo vya afya kwa ajili ya usalama  wao na  watoto wao wachanga.
Imedaiwa kuwa vituo hivyo vya afya, zahanati, hospitali ya rufaa mjini hapa na hospitali ya wilaya ya Iramba, miundo mbinu yake ikiwemo ya maji na ukarabati wa majengo umechangia akina mama wajawazito na  wananchi kukimbia matibabu katika maeneo hayo.
 
IMG_3553Mratibu wa shirika la Riksfobundent For Sexual Upplysning,Jonas Lillberg,akitoa nasaha zake mbele ya mkutano wa wadau wa sekta ya afya,muda mfupi baada ya kukagua utekelezaji wa mradi wa ‘mwanzo mwema’ unaofadhiliwa na shirika la WaterAid likishirikiana na shirika la RFSU ya nchini Sweden.Kushoto kwake ni afisa WaterAid Tanzania Cushbert Maendaenda na kulia ni Jenny Fors kutoka WaterAid makao makuu Sweden.

Mratibu wa Shirika la Kimataifa la Sweden Riksfobundent For Sexual Upplysing (RFSU), Jonas Tillberg ametoa wito huo juzi muda mfupi baada ya kukagua utekelezaji wa mradi wa ‘Wash’ uliokarabati zahanati na miundombinu ya maji katika kijiji cha Mwankoko, uliofadhiliwa na WaterAid Tanzania na RFSU Sweden na kutekelezwa na shirika la SEMA.
Alisema kuwa baada ya yeye na timu yake kutoka nchini Sedwen kukagua miradi wanayoifadhili wamefurahishwa na utekelezaji wake na sasa ombi lao ni walengwa wa mradi kutumia fursa hiyo kikamilifu kwa ajili ya afya zao.
“Wananchi wa Sweden na wafadhili wowote duniani hupenda na hufurahishwa wakiona fedha walizotoa msaada zinawanufaisha walengwa kwa muda mrefu na si vingenevyo,” alisema Tillberg.
Katika hatua nyingine Meneja wa Shirika lisilo la kiserikali la Sustainable Environment Management Action (SEMA), Ivo Manyaku alisema wanatarajia kutumia zaidi ya shilingi 600 milioni kwa ajili ya kugharamia mradi wa ‘Wash’ ambao uboresha  wa sekta ya afya na elimu katika wilaya ya Iramba na Manispaa ya Singida.
Alisema mradi huo  unaendelea kufanya ukarabati  mkubwa katika hospitali ya wilaya ya Iramba na pia vituo viwili  vya afya na baadhi ya shule za msingi katika Wilaya ya Iramba pia kuweka miundombinu ya maji.

IMG_3595Baadhi ya akina mama wakazi wa kijiji cha Mwankoko manispaa ya Singida,wakiwa kliniki iliyopo kwenye zahanati ya kijiji kwa ajili ya watoto wao wachanga kupimwa afya zao.Zaahanati ya Mwankoko ni moja ya vituo vya afya vilivyonufaika na msaada wa zaidi ya shilingi 600 milioni zilizotumika kuboresha miundo mbinu ya maji na ukarabati wa majengo.

“Manispaa ya Singida vile vile  itanufaika na mradi huo kwa kuboreshewa hospital ya rufaa, kituo cha afya cha Sokoine, zahanati ya kijiji cha Mwankoko na baadhi ya shule,” alisema.
Ivo alisema lengo la mradi huo ni pamoja na kumaliza tatizo la uhaba wa maji kwenye vituo vya afya na hospitali  linalochangia maradhi yanayosababisha vifo kwa akina mama wajawazito na watoto wachanga.
Aidha Ivo alisema chini ya mradi huo wanatoa mafunzo kwa baadhi ya watumishi wa idara ya afya yanayohusu usafi wa mazingira, usafi binafsi na utunzaji na namna bora ya matumizi ya miundombinu mbalimbali. 
Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Dkt. Boniface Richard aliwashukru wafadhili wa WaterAid na RFSU kwa kufadhili wa ukarabati mkubwa na uboreshaji wa miundo mbinu ya maji safi na salama kwa hospitali ya wilaya na baadhi ya vituo vya afya.
“Serikali kuu kupitia Wizara yake ya afya imekuwa ikifanya juhudi kubwa kuhakikisha hospitali, vituo vya afya na zahanati zinakuwa na vifaa tiba na madawa lakini suala la maji limekuwa halipewi kipaumbele,” alisema.

IMG_3568Mkurugenzi wa mipango shirika la WaterAid Tanzania,Abel Dugange,akizungumza kwenye mkutano wa hadhara katika kijiji cha Mgongo tarafa ya Shelui wilaya ya Iramba,ambao uliitishwa kwa ajili ya wananchi kupewa ujumbe wa afya ya uzazi na umuhimu wa wananume kushiriki.

Akifafanua Dkt.Richard alisema kabla ya mradi huu unaotekelezwa vema na SEMA, hospitali, vituo vya afya ni zahanati, vilikuwa vinakabiliwa  na uhaba mkubwa wa maji.
Akifafanua zaidi amedai kuwa  kutokana na uhaba huo wagonjwa walilazimika kuleta maji machafu kutoka kwenye madimbwi kitendo kilichokuwa ni hatari zaidi kwa afya zao.
“Maji safi na salama ni muhimu sana kwa ajili ya usafi wa mazingira, usafi binafsi na usafi wa vifaa tiba. Maji yakiwepo ya kutosha kwenye hospitali na vituo vya afya itasaidia sana kupunguza magonjwa yanayosababisha vifo vya akina mama wajawazito na watoto wao wachanga. Niwahakikishie tu ndugu zetu wafadhili kuwa miundombinu hii ya maji iliyoboreshwa na ukarabati wa majengo, tutaitunza na kuilinda kikamilifu,” alisema Mganga huyo Mkuu wa Wilaya.

IMG_3593Meneja wa shirika la SEMA,Ivo Manyaku (wa kwanza kulia) akiwa amepumzika na wafadhili kutoka WaterAid Sweden na wananchi wa kijiji cha Mwankoko nje ya zahanati ya kijiji hicho juzi.Picha na Nathaniel Limu.

IMG_3581Baadhi ya wafadhali wa mradi wa ‘Mwanzo Mwema’ na wananchi wa kijiji cha Mgongo wilaya ya rmba, muda mfupi baada ya kuzinduliwa kwa mradi wa ukarabati mkubwa na uboreshaji wa miundo mbinu ya maji uliofadhiliwa na mashirika ya WaterAid Tanzania na RFSU na kutekelezwa kwa ufanisi na shirika la SEMA.

No comments:

Post a Comment