TTCL

EQUITY

Friday, December 4, 2015

Serikali yaombwa kuzuia sukari za magendo


Afisa mtendaji utawala wa kiwanda cha sukari cha TPC, Jafary Ally.
Hayo yamesemwa na afisa mtendaji wa TPC, Jafary Ally wakati wa ziara ya mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Amos Makala kiwandani hapo ambapo alieleza jinsi namna sukari hiyo inavyoingizwa nchini na jinsi inavyoathiri soko la ndani la bidhaa hiyo.
Bw. Ally amesema kuwa viwanda vya ndani vinadidimia na kushindwa kuendelea kuzalisha kwa faida kutokana na kuingizwa kwa sukari hiyo ambayo huingizwa bila kufuata utaratibu wala kulipiwa kodi.
Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Mh. Amos Makala amesema serikali kwa sasa itajipanga viziri zaidi katika kudhibiti suala hilo ili kuweza kufufua viwanda vya ndani na kuboresha soko la bidhaa hiyo.

No comments:

Post a Comment