Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, UMMY MWALIMU
amevipandisha hadhi vituo viwili vya afya vya MJIMWEMA na MADABA
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, UMMY MWALIMU
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, UMMY MWALIMU amevipandisha hadhi vituo viwili vya afya vya MJIMWEMA na MADABA wilayani SONGEA mkoani RUVUMA, na kuwa hospitali ya wilaya hiyo.
Waziri MWALIMU ametangaza hatua hiyo mkoani RUVUMA wakati wa uzinduzi wa mpango wa huduma za matibabu zinazotolewa na madaktari bingwa uliofadhiliwa na Mfuko wa Taifa wa bima ya Afya - NHIF.
Amesema serikali itaziwezesha hospitali hizo kutoa huduma ya afya kulingana na hadhi stahiki.
Naye Mganga Mfawidhi wa hospitali ya Rufaa ya mkoa wa RUVUMA, Dkt. PHELIS NYIMBI amesema hospitali hiyo inakabiliwa na uhaba wa madaktari.
No comments:
Post a Comment