Nahodha
mpya wa timu ya Taifa ya soka ya Tanzania TAIFA STARS MBWANA SAMATTA
amesema kunahitajika mipango madhubuti ambayo itaimarisha timu hiyo na
sio kuendelea kujaribu kama inavyofanyika hivi sasa
Nahodha mpya wa timu ya Taifa ya soka ya Tanzania TAIFA STARS MBWANA SAMATTA
Nahodha mpya wa timu ya Taifa ya soka ya Tanzania TAIFA
STARS MBWANA SAMATTA amesema kunahitajika mipango madhubuti ambayo
itaimarisha timu hiyo na sio kuendelea kujaribu kama inavyofanyika hivi
sasa.
Akizungumza katika mahojiano maalumu na TBC, SAMATTA amesema TAIFA
STARS imekuwa ikipanda na kushuka na bado haijafika kwenye ubora
unaohitajika.
SAMATTA amesema umefika wakati wa kuwa na mpango mkakati wa
kuipandisha timu hiyo kwa muda mrefu kama vile kuwekeza kikamilifu
kwenye soka la vijana.
TAIFA STARS inayofundishwa na CHARLES BONIFACE MKWASA ina kibarua
kigumu hivi sasa cha michuano ya awali ya kufuzu kwa michuano ya MATAIFA
ya AFRIKA baada ya kutolewa kwenye michuano ya awali ya kuwania kuingia
hatua ya makundi ya kufuzu kwa kombe la dunia.
No comments:
Post a Comment