TTCL

EQUITY

Monday, January 25, 2016

Waomba kasi ya ujenzi wa barabara kuongezwa

Baadhi ya  wananchi na  abiria kutoka mikoa ya GEITA, KAGERA KIGOMA, MWANZA na SHINYANGA wanaotumia barabara ya KIGOMA hadi NYAKANAZI mkoani KAGERA, wameiomba serikali kuongeza kasi ya  ujenzi wa barabara ya  kilomita 50  kwa kiwango cha lami  kuanzia  eneo la KIDAHWE hadi KASULU mkoani KIGOMA, ili kupunguza  adha ya usafiri katika kipindi cha mvua za masika.

 
Wakizungumza katika mahojiano na TBC wananchi hao wamesema katika kipindi hiki cha masika barabara hiyo imekuwa haipitiki kwa urahisi na kusababisha kukwama kwa magari kadhaa ya abiria na  wakati mwingine abiria hulazimika  kulala njiani.

No comments:

Post a Comment